Mkurugenzi wa Elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi Stadi, Prof. Sylivia Temu akizungumza wakati wa uzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS).
 Mkurugenzi wa Elimu ya juu kutoka Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi Stadi, Prof. Sylivia Temu (katikati waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na uongozi wa chuoChuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS), wawakilishi kutokakutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya afya baada yauzinduzi mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kituo hicho kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki na kitakuwa chini ya usimamizi wa  (MUHAS).
Na Mwandishi wetu,
SERIKALI imezindua mradi wa ujenzi wa kituo cha ubora wa sayansi ya magonjwa na mishipa ya moyo hapa nchini kitakachokuwa na uwezo wa kutoa huduma za kitabibu na kitafiti kwenye magonjwa hayo kwa nchi zote za ukanda wa Afrika mashariki.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana kwa niaba ya Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi stadi Bw. Shukuru Kawambwa, Mkurugenzi wa Elimu ya juu nchini, Prof. Sylivia Temu alisema mradi huo unaotekelezwa na serikali kwa ushirikiano na benki ya maendeleo ya Afrika  ni mojawapo ya miradi minne ya afya inayotekelezwa kwenye ukanda wa afrika mashariki ikilenga kutatua changamoto mbalimbali za kiafya.
“Kila nchi ya Afrika Mashariki ina mradi wa aina yake kwenye sekta hii muhimu na kwa upande wetu sisi umejikita katika kukabiliana na magonjwa ya moyo na utakuwa chini ya Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) na utakwenda sambamba na ujenzi wa kampasi mpya ya chuo hicho unaondelea huko eneo la Mloganzila hapa jijini Dar es Salaam,’’ alibainisha.
Akizungumzia faida za mradi huo Prof Temu alisema utasaidia kupunguza vifo vitokanavyo na magonjwa ya moyo hapa nchini sambamba na kupunguza gharama zinazolikabili taifa kwa sasa kutokana na kusafirisha idadi kubwa ya wagonjwa wa moyo kwa ajili ya kutafutaa matibabu nje ya nchi. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...