Umoja wa wanafunzi waliosoma shule ya St Joseph convent school  ya jijini Dar es salaam
iliyodumu kuanzia mwaka 1932 hadi 1969 . Na Forodhani Sekondari  ilyokuwapo kati ya 1970 hadi 2008 ( ilipotaifishwa na serikali) na baada ya hapo St Joseph Cathedral High school 2009 (baada ya kurudishwa kwa kanisa Katoliki)  hadi leo, tumeungana  na kuitwa  St. Joseph & Forodhani  ALUMNI .

St Joseph &Forodhani ALUMNI imeandaa “reunion” mkutano wa pamoja siku ya Jumamosi tarehe 26 September kwa wanafunzi wote waliosoma shule hizo tajwa hapo juu bila kujali umri, jinsi, dini au kabila.

Habari njema, kuna wanafunzi waliosoma shule hii maarufu, wanaoishi nje ya nchi, wanaotoka Canada, Australia, New Zealand Uingereza na Seychelles wanahudhuria mkutano huu wa kishitoria.  Kuna wengine hawajafika Tanzania kwa miaka zaidi ya 30.  Wanarudi kuona shule iliowalea.

Jumamosi tarehe 26 September 2015 kuanzia saa 3 asubuhi kwa shughuli mbali mbali hadi saa 7 mchana katika viwanja vya St Joseph Cathedral High School.
Katika watu maarufu wanaotoka nchi za nje atakuwapo Jaji Mkuu wa mahakama ya Rufaa Seychelles  ambae alisoma hapo na kumaliza kidato cha nne mwaka 1968, na baada ya hapo, kuhamia Seychelles na wazazi wake alipo  kuendelea na masomo ya juu.

Richard Rugimbana                                        Sr Theodora Faustine 
Mwenyekiti wa kamati                                         Mkuu wa Shule





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...