Kikosi kazi cha Timu ya Tanzania Prisons katika Picha ya Pamoja leo katika uwanja wa Sokeine Jijini Mbeya katika Mtanange wa Ligi kuu ya Vodacom Tanzania Bara ambapo Timu ya Tanzania Prison iliibuka mshindi kwa kuwafunga Mbeya City fc Bao moja kwa Sifuri 1-0, ambapo Mchezaji wa Timu ya Tanzania Prison Jumanne Elfadhili dk ya 32 ndiye aliye ipatia ushindi Timu hiyo ya Tanzania Prison baada ya kupokea pande kutoka kwa Salum Kimenya.
Golikipa machachari wa Timu ya Tanzania Prisons Aron Kalambo akiwa amedaka Mpira huku akiwa amezungukwa na Mchezaji wa Timu ya Mbeya City David Kambole Shoto na Wachezaji Salum Kimenya mwenye Jezi Nambari 14 Mgongoni Sanjari na Jumanne Elfadhili..
Mtanange ukiendelea katika Uwanja wa Sokeine Jijini Mbeya ambapo Tanzania Prison iliibuka kidedea kwa kuibugiza Mbeya City fc Goli 1-0.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...