TAARIFA KWA
VYOMBO VYA HABARI
CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kitatoa tuzo kwa Rais
Jakaya Kikwete pamoja na wanamichezo 10 waliofanya vizuri zaidi katika miaka 10
akiwa Rais wa Tanzania.
Tukio hilo ambalo pia litahudhuriwa na Rais Kikwete, litafanyika Oktoba
8, mwaka huu ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam likiwa na lengo la
wanamichezo kumuaga Rais Jakaya Kikwete.
TASWA itakabidhi tuzo maalum kwa Rais ikiwa ni kuthamini mchango wake kwa
maendeleo ya michezo wakati wa miaka 10 ya uongozi wake na imebariki tukio hilo
kama ‘JK na Wanamichezo’.
Licha ya kutoa tuzo kwa Rais na wanamichezo 10 waliofanya vizuri zaidi,
pia TASWA itatoa vyeti maalum kwa kampuni mbalimbali zilizosaidia kwa kiasi
kikubwa kudhamini michezo katika miaka 10 ya Rais Kikwete.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...