IMG_8938
Mwenyekiti wa National Governance Internet Forum ambaye pia ni Rais wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Kenneth Simbaya akiwakaribisha wadau wa mitandao na watumiaji wa intaneti kwenye jukwaa hilo kabla ya kumkaribisha mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA kufungua rasmi jukwaa hilo.. Kulia ni Katibu Mtendaji wa Tanzania Education and Research Network (TERNET), Amos Nungu na Kushoto ni Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph akifuatiwa na Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Bw. Sunday Richard. (Picha zote na Zainul Mzige wa Modewjiblog)
IMG_9076
Picha ya pamoja.

Na Mwandishi Mwetu
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, (UNESCO), limewaomba wadau wa habari hasa wa matumizi ya intaneti kuzingatia maadili na usiri katika kazi zao ili kutovunja sheria zilizowekwa na mamlaka husika likiwemo suala la sheria ya mtandao iliyopitishwa hivi karibuni nchini Tanzania.

Hayo yameelezwa na Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph aliyekuwa akimwakilisha Mkurugenzi wa UNESCO, Zulmira Rodrigues katika Jukwaa la wadau wa usimamizi wa masuala ya mtandao (NIGF), lililofanyika mwishoni mwa wiki na kuandaliwa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...