Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii

KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye (Pichani) amewataka wagombea wa vyama mbalimbali vya siasa kuacha kutumia Udini au Ukanda kutokana na kufanya hivyo ni kuigawa nchi.
  
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Nnauye amesema kuwa kuna watu katika kampeni wamejitokeza kutumia udini na ukanda vitu ambayo ni kinyume na maadili ya uchaguzi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Amesema kuwa baadhi ya wagombea wameonekana katika ibada wakitaka wachaguliwe katika nafasi walizogombea hali ambaya italeta mpasuko wa  udini dhidi ya watu wengine. 

AIDHA Nape amesema kuwa kutokana maadili yaliyotolewa na NEC wagombea wafuate katika kuendesha kampeni ambazo haziwagawi watu.

“Uchaguzi huu watu wasitumie udini au ukanda kwani unagwa watanzania hivyo kila mtu afanye kampeni za kistaarabu na NEC ichukue hatua kwa watu wanaotumia udini”amesema Nape.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Ni wazi kwamba kila mtu afuate taratibu na kanuni zinazokubalika. Angalizo hili ni kwa vyama vyote, kunzia CCM. Nape Nnauye mwenyewe alifanya kosa aliposema kuwa CCM itashinda, hata kwa goli la mkono. Kwangu kama raia ambaye si mwanachama wa chama chochote cha siasa, kauli ile ilikuwa inaashiria shari.

    ReplyDelete
  2. Hakuna sababu ya kugawanya wananchi wa Tanzania.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...