Baadhi ya wakuliwa wa mkoani Shinyanga, wakiwa na maofisa wa Agrics wakati wa mafunzo na uingiaji mkataba wa makubaliano yliofanyika Kijiji cha Ishololo, Wilaya ya Shinyanga Vijijini. Warsha hiyo iliongozwa na Lazaro Japhet (aliyesimama wa tatu kushoto mstari wa mbele. Zaidi ya wakulima 12,000 wanataraji kufaidika na mbegu za mahindi na alizeti kutoka Kampuni ya Agrics.
Mahindi yaliyooteshwa kisayansi na kampuni ya Agrics kwa lengo la kuthibitisha ubora wa mbegu zinazotolewa kwa wakulima wa kanda ya ziwa. Zaidi ya wakulima 12000 watanufaika na mbegu izo msimu huu. Matokeo ya vipimo yalisadifu ubora wa kampuni ya Agrics kwa kutoa asilimia 100% ya ubora.

KUFUATIA msimu mpya wa kilimo unaotarajia kuanza hivi karibuni. Kampuni ya Agrics inatarajia kuwanufaisha wakulima 12,000 wa Shinyanga vijijini, Maswa na Meatu kwa kuwapatia mbegu bora za mahindi, alizeti pamoja na mbolea ili kuhakikisha kilimo biashara kinainuliwa na kuleta tija kwa mkulima. Mbegu hizo zitatolewa hivi karibuni ili kuhakikisha mkulima anakuwa na maandalizi ya uhakika msimu huu. Kampuni ya Agrics hutoa mbegu kwa mkopo nafuu unaolenga kumnufaisha mkulima kwa mazao mengi zaidi.

Pia Agrics ikishirikiana na viongozi wa serikali huwanufaisha wakulima kwa kuwapatia mafunzo katika ngazi tofauti za ukuaji wa mazao ili kuhakikisha mavuno yanasadifu malengo ya wakulima hao.

Akiongea kwa niaba ya kampuni ya Agrics, Meneja Miradi Bw. Charles Laswai alithibitisha ubora wa mradi huo wakati akikabidhi mikataba ya uchaguzi wa mbegu kwa wakulima. ‘’ Ni miaka mitano sasa tangu Agrics ianze kutoa mbegu bora kwa mkopo kwa wakulima wetu wa kanda ya ziwa. 

Kusoma zaidi bofya HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...