Baadhi ya wakuliwa wa mkoani
Shinyanga, wakiwa na maofisa wa Agrics wakati wa mafunzo na uingiaji mkataba wa
makubaliano yliofanyika Kijiji cha Ishololo, Wilaya ya Shinyanga Vijijini. Warsha
hiyo iliongozwa na Lazaro Japhet (aliyesimama wa tatu kushoto mstari wa mbele.
Zaidi ya wakulima 12,000 wanataraji kufaidika na mbegu za mahindi na alizeti
kutoka Kampuni ya Agrics.
Mahindi yaliyooteshwa kisayansi na kampuni ya Agrics kwa
lengo la kuthibitisha ubora wa mbegu zinazotolewa kwa wakulima wa kanda ya
ziwa. Zaidi ya wakulima 12000 watanufaika na mbegu izo msimu huu. Matokeo ya
vipimo yalisadifu ubora wa kampuni ya Agrics kwa kutoa asilimia 100% ya ubora.
KUFUATIA msimu mpya wa kilimo
unaotarajia kuanza hivi karibuni. Kampuni ya Agrics inatarajia kuwanufaisha
wakulima 12,000 wa Shinyanga vijijini, Maswa na Meatu kwa kuwapatia mbegu bora
za mahindi, alizeti pamoja na mbolea ili kuhakikisha kilimo biashara
kinainuliwa na kuleta tija kwa mkulima. Mbegu hizo zitatolewa hivi karibuni ili
kuhakikisha mkulima anakuwa na maandalizi ya uhakika msimu huu. Kampuni ya
Agrics hutoa mbegu kwa mkopo nafuu unaolenga kumnufaisha mkulima kwa mazao
mengi zaidi.
Pia Agrics ikishirikiana na
viongozi wa serikali huwanufaisha wakulima kwa kuwapatia mafunzo katika ngazi
tofauti za ukuaji wa mazao ili kuhakikisha mavuno yanasadifu malengo ya
wakulima hao.
Akiongea kwa niaba ya kampuni
ya Agrics, Meneja Miradi Bw. Charles Laswai alithibitisha ubora wa mradi huo
wakati akikabidhi mikataba ya uchaguzi wa mbegu kwa wakulima. ‘’ Ni miaka mitano
sasa tangu Agrics ianze kutoa mbegu bora kwa mkopo kwa wakulima wetu wa kanda
ya ziwa.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Kusoma zaidi bofya HAPA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...