TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amesema uongezaji virutubisho kwenye vyakula umeibua mguso mpya na kuleta mlipuko baina ya sekta binafsi na sekta za umma (PPP) ambazo zinasimamia masuala ya afya kwa kiwango kikubwa.

Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema kazi kubwa zaidi inabidi ifanyike ili elimu ya kutosha iweze kufikishwa kwa mabilioni ya watu ambao milo yao ya kila siku haina virutubisho vya kutosha.

Ametoa kauli hiyo jana usiku (Jumatano, Septemba 9, 2015) wakati akizungumza na washiriki zaidi ya 400 kutoka nchi 30 wanaohudhuria mkutano wa kwanza wa kimataifa wa urutubishaji vyakula ulioanza jana jijini Arusha. Mkutano huo utamalizika kesho, Septemba 11, 2015.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...