TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
WAZIRI
MKUU Mizengo Pinda amesema uongezaji virutubisho kwenye vyakula umeibua mguso
mpya na kuleta mlipuko baina ya sekta binafsi na sekta za umma (PPP) ambazo zinasimamia
masuala ya afya kwa kiwango kikubwa.
Hata
hivyo, Waziri Mkuu amesema kazi kubwa zaidi inabidi ifanyike ili elimu ya
kutosha iweze kufikishwa kwa mabilioni ya watu ambao milo yao ya kila siku
haina virutubisho vya kutosha.
Ametoa
kauli hiyo jana usiku (Jumatano, Septemba 9, 2015) wakati akizungumza na washiriki
zaidi ya 400 kutoka nchi 30 wanaohudhuria mkutano wa kwanza wa kimataifa wa urutubishaji
vyakula ulioanza jana jijini Arusha. Mkutano huo utamalizika kesho, Septemba
11, 2015.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...