Zaidi ya wanafunzi laki saba 7.7 wanatarajiwa kufanya mtihani wa kumaliza darasa la saba katika vituo zaidi ya elfu 16 nchni nzima kuanzia Septemba 9 hadi 10 mwaka huu. 
 
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Tanzania Daktari Charless Msonde amesema kati ya wanafunzi hao wavulana laki tatu na  sitini na moja elfu sawa na asilimia 45.6, wasichana ni laki nne na kumi na nne elfu sawa na asilimia 53.4, ambapo masomo yatakayotahiniwa ni Kiswahili, Kiingereza, Sayansi, Hisabati na maarifa ya jamii. 
 
Amezitaka kamati za mitihani za mikoa na wilaya kuhakikisha taratibu za mitihani zinazingatiwa ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vituo vya mitihani vinakuwa salama, hususani katika kipindi hiki ambacho baadhi ya viwanja vya shule za msingi vinatumiwa na vyama vya siasa kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Ni kuwatakia wanafunzi wa darasa la saba kote nchini mtihani wa mafanikio.

    ReplyDelete
  2. Yaani nchi nzima ni wanafunzi laki 7 tu?

    ReplyDelete
  3. maisha safari ndefu jamani...dogo ndio wanatupa karata zao.. all the best!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...