NA BASHIR YAKUB -
Unaposhindwa kesi sio mwisho wa kusaka haki. Hii ni kwasababu kushindwa kesi kunatokana na sababu nyingi . Si kweli kuwa kwakuwa umeshindwa kesi katika mahakama fulani basi maana yake ni kuwa ulikuwa huna haki. Yawezekana kabisa haki ilikuwa yako isipokuwa umeshindwa tu kutokana na sababu nyingine za kiutaratibu na kimbinu (procedures & technicalities). Pia waweza kuwa umeshindwa kutokana na uwezo mdogo wa kujieleza na kushindwa kugusa nukta muhimu ambazo kimsingi ndizo zilizokuwa zinabeba shauri lako.
Lakini pia waweza kuwa umeshindwa kwasababu ya hila na mbinu chafu. Na hii wakati mwingine huwahusisha hata waamuzi yaani mahakimu na majaji. Basi ifahamike kuwa ni sababu hizi zilizopelekea kuwepo utaratibu wa rufaa ili yule anayehisi kutotendewa haki aende mbele ili kuona kama anaweza kupata haki yake huko.
1.RUFAA NININI.
Rufaa ni hatua ya kisheria ya kupeleka malalamiko katika hatua ya mahakama ya juu zaidi baada ya mmoja wa wahusika katika kesi iliyoisha kutoridhishwa na hukumu/maamuzi. Ili ukate rufaa ni lazime uwe ulikuwa mhusika katika kesi iliyoisha na uwe na sababu za kwanini unadhani hukuridhishwa na maamuzi. Sababu yoyote ya msingi inakubalika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...