NA  BASHIR  YAKUB -
Unaposhindwa  kesi  sio  mwisho  wa kusaka  haki. Hii  ni  kwasababu  kushindwa  kesi  kunatokana  na  sababu  nyingi . Si  kweli  kuwa  kwakuwa  umeshindwa  kesi  katika  mahakama  fulani  basi  maana  yake  ni  kuwa  ulikuwa  huna  haki. Yawezekana  kabisa  haki  ilikuwa  yako  isipokuwa  umeshindwa  tu  kutokana  na  sababu  nyingine  za  kiutaratibu na  kimbinu (procedures & technicalities).  Pia  waweza  kuwa  umeshindwa  kutokana  na  uwezo  mdogo  wa  kujieleza  na kushindwa  kugusa  nukta  muhimu  ambazo  kimsingi  ndizo  zilizokuwa zinabeba   shauri  lako. 

Lakini  pia  waweza  kuwa  umeshindwa  kwasababu  ya  hila  na  mbinu  chafu. Na  hii  wakati  mwingine  huwahusisha  hata  waamuzi yaani mahakimu  na  majaji.  Basi  ifahamike  kuwa  ni  sababu  hizi   zilizopelekea  kuwepo  utaratibu  wa  rufaa  ili  yule  anayehisi  kutotendewa  haki  aende mbele  ili  kuona  kama anaweza  kupata  haki  yake  huko.

1.RUFAA  NININI.
Rufaa  ni  hatua  ya  kisheria  ya  kupeleka  malalamiko  katika  hatua  ya  mahakama  ya  juu  zaidi  baada  ya  mmoja  wa  wahusika  katika  kesi  iliyoisha  kutoridhishwa  na  hukumu/maamuzi. Ili  ukate  rufaa  ni  lazime uwe  ulikuwa  mhusika  katika  kesi  iliyoisha  na  uwe  na sababu  za  kwanini  unadhani hukuridhishwa  na  maamuzi.  Sababu  yoyote ya  msingi  inakubalika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...