Ndugu Ray Power, ambaye amewahi kuwa Kocha wa Chama Cha Soka na mkuu wa kitengo cha mpira wa miguu katika chuo kiitwacho Central College Nottingham; ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Ufundi katika Kituo cha Vijana cha Michezo kilichopo Kidongo Chekundu jijini Dar es Salaam (pichani). 
Katika nafasi yake mpya, Ndugu Power atasimamia mafunzo na Uongozi wa kituo kipya ambacho kinategemewa kufunguliwa tarehe 19 ya Mwezi huu. Ndugu Power anachukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi wa kituo; Stewart Hall aliyejiunga na timu ya Azam kwa mara nyingine kama Kocha Mkuu.
 “ Hii ni changamoto kubwa kwangu na ninaichukua kwa moyo mkunjufu. Kuna kiwango kikubwa cha elimu kinachoendana bega kwa bega na michezo na sina shaka uzoefu wangu kama kocha na kama muelimishaji ayehitimu mafunzo yake; vyote kwa pamoja vitanipa uwezo unaotakiwa kwenye nafasi hii” alinena Ndugu Power ambaye ni kocha mwenye leseni ya kiwango cha daraja la ‘A’ inayotolewa na Shirikisho la Soka la Ulaya ( UEFA) na mwandishi maarufu wa ukuzaji wa soka la vijana.
Kituo cha Kijamii cha Michezo kitatoa uwanja wa nyasi bandia ulio na ukubwa wa 3G, pamoja na viwanja viwili vinavyoruhusu wachezaji watano watano kila upande, kiwanja kimoja chenye mchanga pamoja na viwanja viwili vya mpira wa kikapu n.k
 Ndugu Power aliongeza “ Filosofia yangu itakuwa kwa mtu mmoja mmoja katika kituo, kumsaidia kila mmoja kuendelea; maana kila mtu ana uwezo wake na udhaifu wake tofauti na mtu mwingine. Nimedhamiria kusaidia ukuaji wa fursa za michezo na njia maalumu za kimpira wa miguu zitakazo wawezesha vijana wa kitanzania kujiandaa kwa changamoto watakazo kabiliana nazo siku za usoni” 
Kituo cha vijana ambacho kimefadhiliwa na Symbion Power, kitapata msaada wa kiufundi na mazoezi kutoka kwa Timu iitwayo Sunderland AFC ambayo inashiriki ligi Kuu ya  Barclays ya Uingereza. Hii itakuwa ya kwanza ya namna yake ya kipekee kwa hapa nchini Tanzania. Maelfu ya vijana wa kitanzania watafaidika na muunganiko wa michezo, elimu na Ushiriki katika Shughuli za kijamii kwa kutumia maarifa na utaalamu wa wakufunzi kutoka timu ya mpira ya Sunderland. 

Paul Hinks, Mtendaji Mkuu wa Symbion Power alinena: “ Kituo cha Vijana Jakaya Mrisho Kikwete ni kiungo cha kati cha Ushirikiano wa kipekee kati ya Symbion Power, Timu ya mpira ya Sunderland na Tanzania na tunaamini ubora alionao Bwana Ray pamoja na uzoefu wa timu ya mpira ya Sunderland utatuwezesha kushuhudia ukurasa mpya wa maendeleo ya michezo nchini Tanzania

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. ni kizuri sana ila kipo mjini sana vijana wetu hawataconcentrate vizuri...kingefaa kupelekwa mkoani au nje ya mji panapo utulivu..vitakavyojengwa vipelekwa nje ya mji

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...