FAMILIA ya Josef Antoni Mloka inatangaza kupotelewa na kijana wao Edimund Josef (Pichani) mwenye umri wa miaka 23 mara ya mwisho aliondoka nyumbani  Julai 3 mwaka huu akiwa amevaa fulana ya rangi ya kijani na modo ya jinsi ya rangi ya bluu tangu siku hiyo tunamtafuta bila mafanikio.
Edimund Josef ni mrefu wa wastani kwa rangi ni maji ya kunde anaupungufu wa akili alikua anaishi Kimara Bonjokwa kwa Mashiringi mtaa wa mjumbe Ally Wila jijini Dar es Salaam. 

Amesoma shule ya Msingi Ukombozi-Mazese alimaliza shule hiyo 2007.

Kwa yeyote atakaye muona sehemu yoyote ile  (Hata kama kwa mtu kwa jirani, jalalani, au akiokota takataka au akiombaomba) tunaomba atoe taarifa kituo cha Polisi cha Urafiki, pia kituo cha Polisi cha Stakishari Ukonga,au kituo chochote cha Polisi kilichopo karibu nawe.
Au unaweza kuwasiliana na Baba mzazi wa kijana huyo Josef Antoni kwa simu namba 0654790019 Au kaka yake Felix Josef  kwa namba 0657536219.
TUNAOMBA USHIRIKIANO WAKO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...