WATANZANIA wametakiwa  kuendelea kudumisha amani hasa kipindi  cha uchaguzi kwani bado nchi yetu inasifika kwa amani dunia kote
kauli hiyo imetolewa na  mwanaharakati wa amani Mhonda Joseph wakati akizungumza na waandishi wa habari jiji Dar es Salaam.

Mhonda amesema wananchi wahakikishe  amani inakuwepo  na hata  wageni wanaoishi hapa  kutokana na historia ya miaka ya nyuma  ya hapa nchini kuwa ya amani.

Aidha  amewataka watanzania wasikubali  baadhi ya watu  wachache kuja kuchochea utovu wa amani na wakumbuke amani ikipotea ni vigumu kuirudisha pindi itakapotoweka.

lakini pia Mhonda ameeleza kuwa  hatua tuliyofikia ya kuwa na vyama vingi  ni moja ya maendeleo  ni mhimu kuhakikisha  tunachagua kiongozi bora  atakao watumikia watanzania wote kutokana na hali ya ugumu wa maisha kwa  sasa.


hata hivyo amewataka mawakala kuhakikisha wanafanya kazi zao bila kukubali kufanya vurugu pindi wanaposimamia wakati wa kuhesabu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...