Bi. Bahati Muriga alifika Ubalozi wa
Tanzania, Washington DC kuhudhuria tafrija iliyoandaliwa na Oxfam America.
Bi. Muriga aliongelea maisha yake katika Mkoa wa Mwanza alipokuwa anafanya kazi
kama Mkuu wa shule ya msingi, pamoja na hayo pia aliweza kuingia katika shughuli za kilimo
akitafuta kipato ya kusomesha watoto wake wawili ili kuwapatia maisha bora.
Ubalozi wa Tanzania Washington DC ulipata ugeni wa wasau kutoka mashirika mbalimbali waliokuja kuungana na Oxfam America inayoandaa Siku ya Chakula Duniani “World Food Day 2015” tarehe 16 Octoba. Bi. Muriga atasafiri kwenda katika mji wa Des Moines, Iowa kushiriki katika ziara na Oxfam inayoandaa matamasha mbalimbali kama ya “World Food Prize”.
Bi Bahati Muriga akielezea ni jinsi gani alivyo na furaha kufika ubalozini na kuweza kukutana na watu mbalimbali kutoka mashirika tofauti hususan OXFAM.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...