THE
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE
OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Miaka
10 inatosha kwa yeyote kutumikia Urais – Rais Kikwete
·
Awataka
watumishi wa Ikulu kumsaidia Rais ajaye kwa ari na nguvu zaidi kuliko
walivyomsaidia yeye.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema
kuwa miaka 10 ya uongozi inatosha kabisa kwa mkuu wa nchi kufanya mambo mengi na
kuwa hahitaji muda zaidi kuweza kumaliza ajenda yake.
Aidha,
Rais Kikwete amewataka watumishi wa Ikulu kumsaidia Rais ajaye hata kwa ari na
nguvu zaidi kuliko hata walimvyosaidia yeye katika miaka yake yote 10 ya
uongozi wake.
Rais
Kikwete aliyasema hayo usiku wa Ijumaa,
Oktoba 16, 2015, wakati alipozungumza na watumishi wa Ikulu katika hafla ya
chakula cha jioni ambako watumishi hao waliagana na Rais Kikwete ambaye
wamemtumikia kwa vipindi tofauti, wengine wakiwa wamekaa naye kwa miaka yote 10
ya uongozi wake.
Akizungumza
na watumishi hao, Rais Kikwete amesema kuwa anaondoka madarakani kwa furaha
sana hata kama anaona huzuni kuagana na watumishi hao wa Ikulu ambao amekaa nao
kwa miaka mingi, baadhi miaka 10.
“Kwa
hakika, naondoka mwenye furaha sana. Ni kweli nasikitika kuwa tunaachana lakini
mambo yote mazuri yana mwisho wake. Nimeifanya kazi ya urais kwa miaka 10, nyie
mnajua aina ya kazi hii.
Miaka 10 ni mingi. Ni miaka inayotosha kabisa kwa mkuu
wa nchi kukamilisha ajenda yake. Sidhani kama mtu anahitaji zaidi ya miaka 10
kutekeleza ajenda yake ya msingi,” amesema na kuongeza:
“Na
hata ukitaka kukaa zaidi huwezi kuyamaliza yote. Mzee Nyerere alikaa miaka 23
hakumaliza yote na yaliyobakia alimwachia Mzee Mwinyi ambaye naye alimwachia
yaliyobakia Mzee Mkapa. Rais Mkapa naye alifanya mengi lakini hakumaliza yote
na akaniachia mimi. Na mimi nitamwachia yaliyobakia Rais ajaye.”
Kuhusu
Rais ajaye ambaye atakuwa mkazi mpya ndani ya Ikulu, Rais Kikwete amesema: “Napenda
kuwaombeni msaidieni sana Rais wetu ajaye. Kwa hakika nawaombeni tumsaidie kwa
ari na nguvu zaidi kuliko hata mlivyonisaidia mimi.”
Imetolewa na:
Kurugenzi ya
Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
19
Oktoba, 2015.
Kila la kheri Rais wetu.Nadhani utapata muda wa "kupumua" sasa maana umeonyesha uvumilivu wa muda mrefu/Ukomavu wa hali ya juu.Urais siyo kazi ya kumjaribisha mtu (moderator usibane comment yangu tafadhali sina nia mbaya)
ReplyDeleteDavid V