Shule ya Sekondari ya WAMA- Sharaf, Mitwero Lindi
Shule ya Sekondari ya WAMA- Nakayama, Nyamisati -Rufiji


Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) inatangaza nafasi za kidato cha kwanza kwa wasichana katika Shule zake mbili za Sekondari:

(1)   Shule ya Sekondari WAMA -  Nakayama  iliyopo Kijiji cha Nyamisati Wilaya ya Rufiji , Mkoa wa Pwani:
(2)   Shule ya Sekondari ya WAMA- Sharaf iliyopo Mitwero katika  Manispaa ya Lindi

WAMA ni Taasisi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa na Mhe. Mama Salma Kikwete ili kusaidia maendeleo ya wanawake na watoto. WAMA inaendesha shule hizi maalum kwa ajili ya watoto yatima na wanaotoka katika mazingira magumu. Hata hivyo, WAMA inatoa fursa chache kwa wanafunzi wengine ambao wazazi wao wana uwezo wa kulipia ili kuongeza uwezo wa kusaidia watoto wengi zaidi. 
Tunafurahi kutoa fursa hii kwa wasichana ambao wataweza kulipia ada kwa kidato cha kwanza katika shule zote mbili kwa mwaka 2016. 
Fomu za kujiunga zinapatikana katika ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Dar es Salaam zilizopo Kawe karibu na Hoteli ya Picolo Beach au katika Tovuti ya Taasisi: www.wamafoundation.or.tz 

Kwa wakazi wa Lindi fomu zinapatikana katika Ofisi za Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) tawi la Lindi zilizopo  katika makutano ya Barabara ya Karume na Amani , Kiwanja no.11 kitalu B karibu na  Ofisi za  Magereza  za Mkoa wa Lindi. 
Kwa Dar es Salaam mtihani wa kujiunga na shule zote mbili utakaotolewa na shule yetu utafanyika Alhamisi Novemba 12, 2015 katika Shule ya Sekondari Jangwani. 
Kwa Lindi mtihani wa kujiunga na shule zote mbili utakaotolewa na shule yetu utafanyika  Alhamisi Novemba 19  , 2015 katika  Chuo cha VETA Lindi.

Mwanafunzi anatakiwa arudishe fomu pamoja na risiti ya malipo katika ofisi za Taasisi ya WAMA au kwa kutumia barua pepe: info@wamafoundation.or.tz, mbugunimwajuma@gmail.com na  alimindria66@yahoo.com.  Mwisho wa kurudisha fomu ni Jumatano tarehe 11 Novemba, 2015. 
Shule zetu zina mazingira na huduma zote muhimu zinazowawezesha wanafunzi kufaulu vizuri yakiwemo mabweni ya kisasa, maabara za kisasa, maabara za computer, maktaba zenye vitabu vya kutosha na walimu wazuri na wakutosha.

Kwa Mawasiliano zaidi:
Piga Namba:  0685-651449, 0789-000341, 0754-439183,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...