Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara, Mhandisi Kato Kabaka (aliyesimama) kutoka Kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania, akitoa elimu ya nishati ya Jotoardhi kwa wafanyakazi wa hifadhi ya wanyamapori Selous na jinsi gani nishati hiyo itaongeza idadi ya watalii.
 Wafanyakazi wa hifadhi ya wanyamapori Selous na kampuni ya uendelezaji wa Jotoardhi Tanzania wakimsikiliza kwa makini Mhandisi Kato Kabaka (hayuko pichani) alipokuwa akiwaelimisha namna nishati ya Jotoardhi itakavyoongeza idadi ya watalii kupitia mabwawa ya kuogelea ya maji moto yatakayojengwa ndani ya hifadhi hiyo.

Bwana Eneck Majahasi (aliyesimama) akihitaji ufafanuzi ikiwa mitambo ya uzalishaji wa nishati ya Jotoardhi itakayojengwa ndani ya hifadhi ya Selous haitakuwa na madhara kwa wanyamapori walioko ndani ya hifadhi.

Na. Lilian Lundo - Maelezo
Kuendelezwa kwa nishati ya Jotoardhi Tanzania itaipelekea kupanda hadhi kwa hifadhi ya wanyamapori Selous.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Mipango na Maendeleo ya Biashara, Mhandisi Kato Kabaka kutoka Kampuni ya Uendelezaji Jotoardhi Tanzania wakati akizungumza na wafanyakazi wa hifadhi ya wanyamapori Selous, kambi ya Matambwe alipokuwa akitoa elimu ya nishati ya Jotoardhi yenye viashiria (majimoto) ndani ya hifadhi hiyo, leo.

“Kama utafiti utaonyesha chanzo cha nishati ya Jotoardhi kipo ndani ya hifadhi, basi nishati hiyo itapelekea hifadhi ya Selous kuongeza idadi ya watalii kwa kujenga mabwawa ya kuogelea yatakayokuwa na maji ya moto na kujenga vibwawa vidogo ndani ya vibanda vya kupumzikia kwa ajili ya kuweka miguu wageni watakao kuwa wakitembelea hifadhi hiyo.” Alisema Mkurugenzi Kato.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...