Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga amewahimiza waandishi wa habari mkoani Dar es salaam kuzingatia maadili ya taaluma hiyo hasa wakati huu ambapo taifa linaingia katika hatua muhimu ya kuchagua viongozi katika uchaguzi mkuu.

Mwamanga ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufungaji wa kongamano hilo amewasihi waandishi wa habari kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia misingi ya taaluma yao ili kuepukana upotoshaji na kuitia nchi katika mgogoro usiokuwa wa lazima. Amesema taaluma ya uandishi wa habari ina umuhimu mkubwa katika kujenga Jamii na isipotumiwa vema inaweza kuhatarisha amani na utengamano wa taifa jambo ambalo amesema halifai kufumbiwa macho.


Zifuatazo ni baadhi ya picha za washiriki wa kongamano hilo lililofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya PEACOCK mjini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bwana Ladislaus Mwamanga akifunga komgamano la waandishi wa habari wa mkoa wa Dar es salaam  lililojadili utekelezaji wa uhuru wa habari kwa uangalifu hususani wakati huu wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu.


Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF bwana Ladislaus Mwamanga (wa kwanza kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa kongamano lililoandaliwa na chama cha waandishi wa habari mkoa wa Dar es salaam baada ya kufunga rasmi kongamano hilo lililojadili juu ya uchaguzi huru na haki bila waandishi wa habari kuzingatia maadili ni ndoto. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...