UN 1
Katibu Mkuu wa Baraza la Mahedhebu kwaajili ya Amani,Mchungaji,Canon Thomas Godda akizungumza katika kongamano la Amani lililoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu,Sayansi na Utamaduni (UNESCO)kwa kushirikiana na madhehebu ya Dini na Viongozi wa Mila ili kuhamasisha amani katika kipindi cha uchaguzi na baada ya uchaguzi.

Na Mwandishi wetu, Simanjro
Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia na Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) limekutanisha wadau mbalimbali katika kongamano la kujadili na kuhamasisha amani katika kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba 4,2015.

Kongamano hilo lilifanyika katika Kituo cha Redio Orkonerei (ORS)Terrat wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara na kuwaleta pamoja viongozi wa dini,mila na wawakili wa muungano wa Redio za Jamii nchini(Comneta)ambao kwa pamoja walisisitiza umuhimu wa amani.

Ofisa Miradi ya Mawasiliano, Habari na Tehama wa Shirika la Kimataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni (UNESCO) nchini, Al Amin Yusuph alisema mchango wa unaotolewa na Redio za kijamii nchini ni mkubwa kwani unawawezesha wananchi kuzitumia kujiletea maendeleo katika nyanja mbalimbali ikiwemo ya kuhamasisha amani na utulivu katika kipindi hiki na baada ya uchaguzi mkuu.

Ameongeza kuwa Muungano wenye nguvu wa Redio za Jamii ndio ukombozi wa wananchi kwani wanahitaji kuelimishwa maswala mbalimbali ya afya, kilimo na programu zinazoandaliwa na serikali kwajili ya wananchi.

Mmoja wa viongozi wa mila ,Laigwanani Lesira Samburi alisema viongozi wa mila licha ya mchango wao kwenye jamii bado hawajashirikishwa ipasavyo pamoja kuwa huwa hawajishughulishi na siasa moja kwa moja.

"Naomba serikali itambue mchango wetu katika kutatua migogoro na kuhamasisha amani kwenye jamii zetu,tunaweza kufanya mambo makubwa kama serikali ikitushirikisha ipasavyo sio katika kipindi hiki cha uchaguzi tu bali hata baada ya uchaguzi,"alisema Samburi
UN 2
Mwenyekiti wa Radio za Jamii kutoka UNESCO na Mhadhiri Mwandamizi wa Mawasiliano katika Chuo Kikuu cha Hyderabad, Profesa Vinod Pavarala akizungumza katika kongamano la amani, lililofanyika katika Kituo cha Redio ya Jamii ya ORS (OPA)iliyopo wilaya ya Simanjiro mkoa wa Manyara. Pichani wanaofatilia kwa karibu ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Dini kwa ajili ya Amani, Mchungaji Thomas Godda na Afisa Miradi wa UNESCO, Al-Amin Yusuph.

KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...