Na Ally Daud-Maelezo

Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa wito kwa vijana kutojihusisha na vitendo vya fujo katika kipindi hiki cha  kampeni  badala yake waelekeze nguvu na  juhudi  zaidi katika kujenga uchumi wa taifa.
Akiongea katika mkutano uliowakutanisha NEC na wawakilishi wa vijana kutoka mikoa mbalimbali nchini Makamu Mwenyekiti wa Tume, Jaji mkuu Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Hamid Mahmoud Hamid  (pichani) alisema kuwa  vijana wasitumike na vyama vya siasa kama kichocheo cha fujo .

“Vijana kamwe msikubali kutumika kwa maslahi ya chama cha siasa ila tumieni vizuri elimu yenu na upeo wenu wa kufikiri namna ya   kujenga na kuendeleza  taifa”,alisema Jaji Hamid.
Aidha Jaji Hamid aliongeza kuwa vijana wanapaswa kuhamasisha watu mbalimbali umuhimu wa kupiga kura kwani wao ni sehemu muhimu na ndiyo nguvu pekee inayotegemewa katika jamii ya Tanzania.
Naye  Mkurugenzi wa NEC  Bw. Kailima Ramadhan amesema kuwa  wananchi wanatakiwa kuheshimu  sheria na kanuni za uchaguzi  kwa  mwaka  huu wa 2015 ili kufanya uchaguzi kuwa haki na amani.
“ Natoa wito kwa wananchi  wa Tanzania  kuepuka  kuingilia kazi za watumishi wa Tume ya uchaguzi kwa kuhakikisha kuwa kila mwananchi atapiga kura katika kituo alichojiandikisha ili kuepusha usumbufu “ alisema Bw. Ramadhan .

Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeweka utaratibu maalum wa namna ya  kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika  Octoba 25 mwaka huu kwa  ngazi ya Rais, Wabunge na Madiwani ambapo madiwani watatangazwa na mkurugenzi wa NEC ngazi ya kata, Wabunge ngazi ya Jimbo na Rais atatangazwa na Tume ya Uchaguzi (NEC).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...