Msajili wa Vyama vya  Siasa Jaji Francis Mutungi  akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya   utofauti wa itikadi wa vyama ndiyo ukomavu wa demokrasia nchini hivyo ni jambo la busara kuvumiliana na kufanya siasa za kistaarabu, ameyasema hayo wakati  wa  kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam kulia ni Balozi wa Amani Mrisho Mpoto na kushoto ni Balozi wa Amani Christina Shusho.
 Balozi wa Amani Mrisho Mpoto akifafanua jambo katika kikao hicho leo jijini Dar es Salaam.
 Msajili wa Vyama vya  Siasa Jaji Francis Mutungi, katika kikao kilicho fanyika leo jijini Dar es Salaam.
(Picha na Emmanuel  Massaka)

Na Magreth Kinabo-maelezo
OFISIya Msajili wa Vyama  Vya Siasa imewaasa na kuwataka viongozi wote wa  vyama  vya siasa kutoa kauli na maelekezo kwa wafuasi wao na wanachama wa vyama vyao kutoshiriki katika aina yoyote ile ya uvunjifu wa amani hususan katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu na baada  ya uchaguzi huo.

Hayo yamesemwa  leo na Msajili wa Vyama Vya Siasa, Jaji Francis Mutungi wakati akizungumza na waandishi wa habari leo kwenye ukumbi wa mikutano uliopo katika ofisi hiyo jijini Dares Salaam.

“Dhamana  ya nchi iko mikononi mwenu,ushawishi wenu kuhusu amani katika kipindi hiki ndio utakaoliokoa taifa la Tanzania ama  utaliingiza taifa katika vurugu na mfarakano,” alisema Jaji Mutungi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...