Meneja mauzo Kanda ya Kaskazini wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, Aluta Kweka ( kulia) pamoja na Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Hafsa Mtasiwa (wa kwanza kushoto) akifatia na Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe Patricia Andrew Mbigili (katikati) wakiwa na baadhi ya wanafunzi wa shule ya sekondari ya mazinde Day wakionyesha vitabu walivyokabidhi na Airtel ikiwa na lengo la kutatua changamoto ya uhaba wa vitabu shuleni hapo. Vitabu hivyo vya sayansi vinathamani ya shilingi milioni 3. 

KAMPUNI ya simu ya mkononi ya Airtel kupitia mpango wake wa Airtel shule yetu imetoa msaada wa vitabu vyenye thamani ya sh.milioni tatu kwa Shule ya Sekondari ya mazinde Day ya mkoani wa Tanga wilaya ya Korogwe.

Akikabidhi msaada huo jana Meneja mauzo Kanda ya Kaskazini Aluta Kweka alisema kuwa kwa kutambua umuhimu wa kuendeleza elimu nchini Airtel ililazimika kuanzisha mpango huo ili kuongeza viwango vya ufaulu.

Alisema kuwa vitabu vilivyotolewa ni vya sayansi hivyo kupitia vitabu hivyo wanafunzi wataongeza bidii kwa kuvisoma na kusaidia idadi ya wanafunzi wanaofaulu katika masomo hayo ambayo awali ilionekana ni masomo magumu kutokana na kutokuwa na vitendeakazi.

Alisema kuwa utoaji wa vitabu hivyo kwa shule za sekondari ni mmrefu unaofanywa na kampuni yake ili kutimiza dhamira yake ya kurudisha faida wanayopata kwa Watanzania na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii.
Meneja mauzo Kanda ya Kaskazini wa Airtel, Aluta Kweka akimkabidhi vitabu vya sayansi mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari Mazinde Day, Bi Jermana Mchome (katikati) ikiwa ni msaada katika kuendeleza elimu na kutatua changamoto za uhaba wa vitabu shuleni hapo. Akishuhudia ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe,Hafsa Mtasiwa. 

Alisema kuwa hadi sasa zaidi ya shule 1,300 zimenufaika na mradi huo ambapo umechangia kupunguza changamoto ya ukosefu wa vitabu kwa shule zilizokabidhiwa.

Akizungumza wakati wa kupokea msaada huo Mkuu wa wilaya ya Korogwe Hafsa Mtasi aliipongeza kampuni hiyo ambapo imekuwa ikisaidiana na serikali katika kuinua kiwango cha elimu nchini.

"Tunaipongeza Airtel kwa mpango huu kwani umekuwa ukichangia kupunguza changamoto ya ukosefu wa vitabu katika shule za sekondari na ni mfano mzuri wa kuigwa," alisema.

Naye Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya Mazinde Day,Jermana Mchome aliishukuru Airtel pamoja na kuwasisitiza wanafunzi wa shule zote zilizofaidika kuvitumia vitabu kikamilifu ili kujiendeleza kwa manufaa ya jamii zao pamoja na taifa kwa ujumla.

"Sasa ni jukumu lenu wanafunzi kutumia fursa hii kusoma kwa bidii ili muweze kusaidia taifa baada ya kisomo chenu, msaada huu mkiutumia vizuri ni nyenzo kubwa sana yakusaidia hata familia zenu kutokana na faida kubwa mtakayopata kutokana na zao la elimu” alisema.

Kampuni ya simu ya Airtel imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia sekta ya elimu kupitia mpango wake wa Airtel Shule Yetu bado inasaidia vijana mbalimbali hapa nchini kutatua changamoto mbalimbali kupitia mradi wake mpya wa Airtel FURSA Tunakuwezesha
Meneja mauzo Kanda ya Kaskazini wa Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel, Aluta Kweka (kushoto) pamoja na Mkuu wa wilaya ya Korogwe ,Hafsa Mtasiwa na Mwalimu Mkuu wa shule ya sekondari ya Mazinde Day, Jermana Mchome (katikati) wakionyesha vitabu walivyokabithi na Airtel ikiwa na lengo la kutatua changamoto ya vitabu shuleni hapo. Vitabu hivyo vya sayansi vinathamani ya shilingi milioni 3.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...