Na Lorietha Laurence-Maelezo

Bodi ya Korosho Tanzania imeadhima kutoa asilimia 7 ya mapato yake sawa na shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kusaidia utafiti wa zao hilo unaofanywa na kituo cha utafiti cha Naliendele.

Akiongea wakati wa kufunga kwa mkutano wa tatu wa kimataifa uliowahusisha wadau kutoka nchi mbalimbli duniani ,Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Korosho Tanzania Bw. Muhidhiri Muhidhiri amesema kuwa changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni ukosefu wa fedha kwa ajili ya kuendeshea utafiti wa zao la korosho unaofanywa na kituo cha Naliendele na hivyo wamejipanga kwa kuchangia kiasi cha mapoto ili kufanikisha tafiti hizo .

Muhidhiri aliongeza kuwa licha ya changamoto za ukosefu wa fedha wamepata fursa ya kujifunza mambo mbalimbali kupitia mkutano huo ikiwemo maadhimio ya uzalishaji bora wa zao hilo, namna ya kutatua matatizo ya magonjwa yanayoikumba korosho,dawa asilia zitakazosaidia katika kulinda mbegu, na njia bora ya uzalishaji.

“Mkutano ulikuwa wa kisayansi kwa kuwa umeangalia mambo ya kiutafiti na teknolojia katika uzalishaji wa zao la korosho hivyo ninaamini baada ya hapa ni kuanza utekelezaji wa yale tuliyoyajadili na kufanya vizuri zaidi ” alisema Muhidhiri.



Kwa upande wa Mtafiti Mkuu wa Masuala ya korosho Prof.Peter Masawe ameeleza kuwa mkutano huo wa wadau umewapa fursa ya kufahamu mambo mazuri katika uboreshaji na uzalishaji wa zao la korosho katika kiwango kizuri na kilicho bora .

Pia alibainisha kuwaTanzania ndiyo nchi yenye mtafiti anayetegemewa katika masuala ya korosho na hivyo kupitia mkutano huo wadau wamepata fursa ya kufahamu mambo ya msingi kama vile mbegu bora zinazozalishwa nchini ,mbegu fupi, mbegu zinazostahimili ukame pamoja na kukopa teknolojia ya uzalishaji.

“Mkutano huu umetoa fursa kwa wadau kujua mambo muhimu kuhusu mbegu ukizingatia Tanzania ndiyo nchi pekee barani Afrika inayozalisha mbegu bora hivyo natumai wajumbe wataenda kutendea kazi yale yote waliyojifunza hapa kwetu na nasisi pia tutayafaniya kazi yale tuliyoyapata kutoka kwao ” alisema Prof Masawe.

Mkutano huo wa kimatifa wa wadau wa Korosho umefanyika kwa mara ya pili nchini ambapo mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1997 na hivyo kuipa fursa nchi ya kujitangaza kupitia sekta ya kitalii kwa kuwahamasisha wadau waliohudhuria mkutano huo kutembelea sehemu za vivutio ikiwemo Bagamoyo na Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...