Kampuni ya mawasiliano ya simu za mkononi Airtel  leo imefungua duka jipya na la kisasa  mjini Moshi lililopo katika mtaa wa Soko Kuu. Uzinduzi wa duka hili linadhihirisha ahadi yake kwa Airtel kujali wateja wake Tanzania nzima na kuwapa huduma iliyobora na ya kiwango cha juu popote pale walipo.

Hii ni sehemu ya mpango wa kampuni hiyo kuhakikisha wanatoa na kuboresha  mpango wake wa huduma kwa wateja wake  ili kuongeza urahisi wa kuwafikia wateja wake mbalimbali popote pale walipo nchi nzima.

Akizungumza katika sherehe fupi ya ufunguzi wa duka hilo,mkurugenzi  wa kitengo cha huduma za wateja wa Airtel, Bi Adriana Lyamba, alisema kuwa ufunguzi wa duka hili jipya na la kisasa mjini Moshi ni mwendelezo wa malengo ya Airtel kuendeleza  kuboresha maisha morani kwa kila mtanzania kwa kupata huduma zenye zenye ubora na kuwafikia wateja kwa urahisi zaidi popote walipo.

"Tunafuraha kubwa sana kuona tunafanikiwa kuwafikia wateja wetu na kufungua milango kwa wateja zaidi mjini Moshi na kuwahakikishia kuwa    tunafanya ubunifu wa hali ya juu wa kiteknolojia ili kutumia mtandao wa simu kuboresha maisha ya wananchi ikiwemo kutoa huduma bora na ndio maana tunazidi kufungua maduka kama haya kwa ajili ya kuwasogezea huduma  karibu na wananchi, na ninawahakikishia kuwa popote wateja wetu walipo tutawafikia , "alisema Lyamba

Duka hili jipya  lenye mazingira mazuri kwa wateja litakuwa linatoa huduma mbalimbali kwa wateja wa Airtel ikiwemo huduma za modem, Airtel Money, simu mpya za kisasa za smartphone, huduma zetu za intanet na huduma ya malipo ya bili za awali na mwezi .

               
Bi, Evelyne Zakaria ambae ni Afisa tarafa wa Moshi Mashariki kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Moshi, Novatus Makunga aliwashukuru Airtel kwa dhamira yake ya  uboreshaji wa huduma kwa wakazi wa mji wa Moshi. Pia alibainisha kuwa mawasiliano ni jukumu kubwa katika kuunganisha watu na biashara ya kuendesha maendeleo katika Kata ya Moshi.

Mkuu wa Wilaya aliyaomba makampuni mengine ya simu yajitokeze zaidi na kuiga mfano wa Airtel  katika kutoa huduma bora kwa wakazi wa mji wa Moshi akisema kuwa ofisi yake iko tayari kwa kutoa ushirikiano kwa lengo la kufanya maisha bora kwa wakazi wake.
Toka kushoto ni Meneja wa mamlaka ya mawasiliano kanda ya kaskazini (TCRA) Eng, Annette Mahimbo Matindi na Afisa tarafa wa Moshi Mashariki bi Evelyne Zakaria (kati) wakiwa na Mkurugenzi wa huduma kwa wateja wa Airtel Bi, Adriana Lyamba wakishirikiana kukata utepe wakati Airtel ikizindua duka jipya mkoani Kilimanjaro mtaa wa Mandela jana. Kulia wakwanzani akishudia ni Meneja wa Biashara wa Airtel kanda ya kaskazini bw Brighton Majwala.
Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Airtel Tanzania, Bi. Adriana Lyamba akijadiliana jambo na Meneja wa tawi la Biashara la Airtel Mkoa Kilimanjaro, Bw. Paschal Bikomagu (kushoto) na msimamizi wa maduka hayo bw, Thomas Chalamila mara baada ya Airtel kuzindua duka la kisasa moshi mtaa wa mandela jana au soko kuu.
Mkurugenzi wa Huduma kwa wateja wa Artel, Bi. Adriana Lyamba akimuhudumia Mteja aliefika kwenye duka hilo, Bw. Ally Janja ambae ni Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Kilimanjaro na pia mmoja kati ya wateja maalum wa Airtel wakiwa katika duka jipya la Airtel Moshi lenye kona maalum kwa wateja hao (Airtel Premium) mara baada ya duka hilo jipya na lakisasa kufunguliwa jana na Airtel mkoani Kilimanjaro.
Picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...