Na Bashir Yakub
Serikali  mpya  imeanza  kwa  kasi  kubwa kufuta  umiliki  wa  viwanja  nyumba na  kubomoa  yale  maeneo  yote  wanayoona  hayastahili. Upo  umuhimu  wa  kujua  namna  ya  kuepuka  kuingia  katika  janga  hili.

1.Kifungu cha 45 (2)(i-vi) cha Sheria ya Ardhi kinaeleza sababu za msingi zinazoweza kusababisha mhusika kubomolewa, kufutiwa umiliki ardhi kama ifuatavyo :
( a ) Kwanza iwapo eneo limetelekezwa kwa muda usiopungua miaka miwili. Muda usiopungua miaka miwili maana yake ni kuanzia miaka miwili na kwenda mbele. Kutelekeza eneo kwa mujibu wa maana hii hapa ni pamoja na kutoonekana ukishughulika na eneo lako kwa namna yoyote tangu upatiwe umiliki.
( b ) Jaribio lolote la kutaka kuuza au kugawa ardhi kwa mtu asiyekuwa Mtanzania. Ni kosa mtu asiyekuwa raia wa Tanzania kumiliki ardhi, hivyo jaribio lolote la kumpatia ardhi linatosha kuwa kosa la kufutiwa umiliki.

( c ) Epuka  kujenga  maeneo  ya  wazi, maeneo  yaliyotengwa  kwa  ajili ya  miundo  mbinu, na  huduma  nyingine  za  umma. Kufanya  hivyo  hutafsiriwa  kama  kuukosesha  umma  manufaa  yaliyokusudiwa  na  ni  kinyume  na tamko  namba 6.6.1 la  sera  ya  taifa  ya  ardhi  ya  mwaka 1995.

 ( d ) Jaribio lolote la kutoa ardhi kwa mamlaka nyingine kinyume na namna ulivyoagizwa na mamlaka wakati unapewa eneo husika.
(  e  ) Kutumia eneo kinyume na masharti yaliyo kwenye hati ikiwa ni pamoja na matumizi yoyote yaliyo kinyume na sheria ya ardhi, sera, miongozo na kanuni zake.
(  f  ) Pia, Rais kwa mamlaka aliyonayo, anaweza kufuta umiliki wa ardhi ya mtu yeyote kwa sababu zozote zinazohusu maslahi ya umma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...