KWAYA  ya  Wakorintho  wa Pili ya Wilayani Mafinga mkoani Njombe, imekuwa ya kwanza  kuthibitisha kushiriki Tamasha la Kushukuru linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama alisema uongozi wa kwaya hiyo umekubali kushiriki katika tamasha hilo baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 nchini kote.

“Kwaya  ya Wakorintho wa pili  wameanza kuthibitisha kushiriki tamasha la Shukrani baada ya kufanyika uchaguzi Mkuu kwa amani na utulivu, tunaendelea na maandalizi ya kufanikisha tamasha hilo ambalo litashirikisha idadi kubwa ya Watanzania,” alisema Msama. 

Aidha Msama alisema katika tamasha hilo, Kwaya hiyo itafanya uzinduzi  wa albamu yake ya Mchepuko sio dili yenye nyimbo nane.Nyimbo zilizoko kwenye albamu ya Mchepuko sio dili ni pamoja na Tanzania, Mchepuko sio dili, Watenda mabaya, Eee bwana, Tuokoe baba, Dunia hii, Yahwe Tunakuinua na Hana.  

“Kwaya  ya Wakorintho itafanya matukio mawili katika tamasha hilo, la kwanza ni kushiriki Tamasha la Kushukuru na la pili ni kuzindua albamu yenye nyimbo nane,” alisema Msama. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...