Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (Kulia), akitoa hotuba wakati wa mahafali ya nne ya Shule ya Sekondari Louis Montfort, iliyoko Yombo jijini Dar es Salaam Novemba 21, 2015. Maleta ambaye alikuwa mgeni rasmi kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu, alisema TAA inafarijika sana kushirikiana na jamii iliyo jirani na viwanja vyake vya ndege kote nchini na kwamba itasaidia kutatua baadhi ya changamoto zinazoikabili shule hiyo ili kuendelea kushirikiana katika kutunza uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.

Mkurugenzi wa Sheria wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, (TAA), ambaye pia anashughulikia Mahusiano, Ramadhan Maleta, (wapili kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na mwanafunzi wa kidato cha nne ambaye amefanya vizuri kwenye masomo ya kuhitimu kidato cha nne, Emmy Bisco Duma, (watatu kushoto), wakati wa mahafali ya nne ya Shule ya Sekondari Louis Montfort iliyoko Yombo jijini Dar es Salaam Novemba 21, 2015. Wengine kutoka kushoto ni viongozi wa Shule hiyo, Jimmy George, Mkuu wa Shule, Jim Madavana, na Mkuu wa Taaluma, Chiku J. Sekilasi.
(Picha Kwa Hisani ya TAA)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...