Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli anamtumia salamu za rambirambi Mwenyekiti wa Chama Cha Madereva Tanzania (TADWU) kufuatia kifo cha aliyekua Katibu Mkuu wa Chama hicho Bw. Rashid Salehe kilichotokea Tarehe 20 Novemba, 2015 katika Hospitali ya Taifa Mhimbili.

Katika salamu hizo Rais Magufuli amesema taifa limempoteza mtu shupavu, mkweli, makini na aliyependa kupigania haki pale alipoamini kuwa panastahili haki hiyo na alithibitisha kwa kupigania uanzishwaji wa Chama Cha Madereva na kusimama kidete kutetea haki zao.

"Nawatakia moyo wa uvumilivu familia ya marehemu, ndugu, jamaa, marafiki,  madereva na wengine wote ambao wameguswa na kifo cha Rashid Salehe na wote tuungane kumuombea kwa Mwenyezi Mungu ampumzishe mahali pema peponi".

marehemu Rashid Salehe enzi za uhai wake.

Dr Magufuli anaungana na wote walioguswa na msiba huo katika kipindi hiki kigumu na kwamba taifa litauenzi mchango mkubwa alioutoa marehemu Rashid Salehe.

Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi Mawasiliano, IKULU
23 Novemba, 2015.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...