Na Kaka Mwinyi
Kundi mahiri kabisa la muziki wa mahotelini, Mambo Afrika lenye maskani yake huko Dubai, Falme za Kiarabu, limezidi kujipngezea umaarufu baada ya kutajwa katika orodha ya ‘Waburudishaji Bora’ wa mwaka.
Kundi hilo linaloundwa na wasanii kadhaa toka Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, limeingizwa katika orodha ya wadau wa masuala ya burudani nchini humo kutokana na uwezo wake wa kuburudisha katika maonesho mbalimbali linapoalikwa.
Mmoja wa viongozi wa kundi hilo, Giovanni King (pichani kulia), amesema kuwa, Mambo Afrika inajivunia hatua hiyo aliyoilezea kuwaimarisha zaidi kwa kufanya kazi nzuri na bora kila kukicha katika kukabiliana na ushindani mkubwa uliopo kwa bendi na vikundi vya sanaa vinavyotumbuiza sehemu mbalimbali huko Dubai.
“Kundi letu lina wasanii wachache sana. Tunaye muimbaji wa kike Winfrida Masi ‘Winnie’, mpiga gitaa la besi Philip Kazamir na Miraji Chocholi anayecharaza drums. Wengine ni wapapasa vinanda Angelus Lyampawe na Johannes Lista na mimi mwenyewe (Giovanni). Tuko vizuri sanjari na wanenguaji (dancers) ambao huwa tunawabadilisha mara kwa mara kulingana na mahitaji ya nyakati,” akasema Giovanni.
Aidha, Giovanni aliyewahi kutamba na bendi ya Chuchu Sound miaka ya mwanzoni ya 2000, amesema Mambo Afrika hufanya maonesho yake kwenye klabu ya kimataifa ya Africana iliyopo ndani ya hoteli ya Palm Beach ambayo iko kitongoji cha Bur-Dubai.  Katika maonesho yake, Mambo Afrika hupiga muziki wa aina zote.
 Kundi mahiri kabisa la muziki wa mahotelini, Mambo Afrika lenye maskani yake huko Dubai, Falme za Kiarabu

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Men in african, girls in western.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...