Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
SHIRIKISHO la Wasanii nchini  wamewataka mashabiki wao kuondoa tofauti  za kiitikadi ambazo zilijitokeza  katika kampeni waendelee kuwaunga mkono.

Akizungumza na waandishi wa habari,mmoja wa msanii, Stara Thomas amesema kila watu walikuwa na itikadi katika kampeni hivyo ni wakati mwafaka wa kufanya kazi.

Stara amesema wameshiriki katika kampeni zimeisha sasa ni wakati kushiriki katika majukumu kama wasanii.

Hata hivyo amesema wanapongeza Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Pombe Magufuli kwa kuchaguliwa na watanzania  katika kuongoza.

Nae Msanii Mkongwe, John Kitime amemtaka Rais kuwekea umuhimu wa idara ya utamaduni  kuweza kufanya wizara kutokana na kuwepo kwa changamoto nyingi kwa wasanii.

Kitime amesema idara hiyo kuhama hama kumewafanya wasanii kuwa nyuma na kufanya nchi kushindwa kupata mapato licha ya wasanii kuwa wengi.

Kwa upande Mkurugenzi wa Bendi ya Twanga Pepeta, Asha Baraka ameshauri Rais mpya katika uteuzi wa bodi wasanii wateuliwe kutokana na uwezo wao katika kazi hiyo.

Asha amesema kuteuliwa kwa wasanii katika bodi zenye sanaa nchini zitaleta chachu na wasanii watatambuliwa na jamii kwa mchango wao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...