Leo usiku ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni kutakuwa
na tukio kubwa la kiburudani ambapo Mashauzi Classic Modern
Taarab, watazindua albam yao mpya ya “Sura Surambi”.
Uzinduzi wa albam hiyo iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa,
utasindikizwa na kundi kongwe la taarab - East African Melody.
Mkurugenzi wa Mashauzi Classic, Isha Mashauzi ameiambia JAMBO
LEO kuwa albam ya “Sura Surambi” inaundwa na nyimbo sita kali.
Isha amezitaja nyimbo hizo kuwa ni pamoja na “Sura Surambi”
aliouimba yeye, “Kupendwa Bahati Yangu” uimbaji wake Abdumalick
Shaaban, na “Mjinga Mpe Cheo” wa Zubeida Malick.
Nyimbo nyingine alizozitaja Isha ni “Pendo la Ukakasi” wa Saida
Ramadhan, “Ubaya Haulipizwi” ulioimbwa na Asia Mzinga na
“Mapenzi Yamenivuruga” mwimbaji akiwa ni Naima Mohamed.
Nyimbo zote hizo sita zimetungwa na Isha Mashauzi.
Mbali na East African Melody, mkali wa tungo za mahaba Cassim
Mganga naye pia atasindikiza uzinduzi huo wa albam ya “Sura
Surambi”.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...