Hatimaye albam ya “Sura Surambi” iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa taarab, inazinduliwa Alhamisi hii Novemba 26.

Albam hiyo kutoka kwao Mashauzi Classic, itazinduliwa ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni huku kundi kongwe la taarab East African Melody, likizindikiza tukio hilo kubwa.

Mkurugenzi wa Mashauzi Classic, Isha Mashauzi ameuambia mtandao huu kuwa albam ya “Sura Surambi” inaundwa na nyimbo sita kali.

Ni Alhamisi ya kihistoria ambayo Isha anaitaja kuwa itapambwa na ratiba iliyokwenda shule itakayomwacha mshabiki apate uhondo mwanzo mwisho.

Isha amezitaja nyimbo hizo kuwa ni pamoja na “Sura Surambi” aliouimba yeye, “Kupendwa Bahati Yangu” uimbaji wake Abdumalick Shaaban, na “Mjinga Mpe Cheo” wa Zubeida Malick.

Nyimbo nyingine alizozitaja Isha ni “Pendo la Ukakasi” wa Saida Ramadhan, “Ubaya Haulipizwi” ulioimbwa na Asia Mzinga na “Mapenzi Yamenivuruga” mwimbaji akiwa ni Naima Mohamed.

Nyimbo zote hizo sita zimetungwa na Isha Mashauzi.

Mbali na Melody, mkali wa tungo za mapenzi wa muziki wa kizazi kipya Cassim Mganga naye pia atasindikiza uzinduzi huo wa “Sura Surambi” ndani ya Mango Garden Alhamisi hii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...