(Jovina Bujulu-MAELEZO)
 
Sekta ya ardhi nchini ni ya kipekee katika uthibiti wa mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwa ndiyo sekta pekee ambapo ndipo uzalishaji na uondoaji wa kaboni hutokea.

Mfumo wa matumizi mapana ya ardhi ambao siyo endelevu unapaswa ubadilishwe ili nafasi yake ichukuliwe na matumizi ambayo ni sahihi na endelevu zaidi tofauti na hali ilivyokuwa mwanzo. Hatua hiyo ni pamoja na kutumia vyema ardhi iliyopo kwa kupunguza uzalishaji wa gesi joto unaotokana na ardhi.

Mnamo mwaka 2009, Ubalozi wa Ufalme wa Norway nchini Tanzania ulianza kuwa chachu ya uhifadhili wa miradi saba ya majaribio ya Mkakati wa Kupunguza Ukataji Hovyo  na Uharibifu wa Misitu (MKUHUMI) kwa kutoa dola za Kimarekani zipatazo milioni 100 kufadhili mradi huo.

Fedha hizo zilipelekwa kwenye taasisi za elimu ya juu nchini ambazo zinajukumu la kuandaa wataalamu mbalimbali.
Taasisi zilizopata fedha hizo ni pamoja na Chuo Kukuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwa lengo la kuendesha mafunzo na utafiti.

Fedha nyingine zilipelekwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, kitivo cha Tathmini ya Rasilimali ambako huko pia waliingia mkataba na Asasi zisizo za Kiserikali (NGO’s) za hapa nchini ili kutekeleza mkakati wa MKUHUMI vijijini.

Mkurugenzi wa Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt Julius Ningu hivi karibuni alibainisha kuwa MKUHUMI ni moja ya maeneo ya utekelezaji wa mkataba wa mabadiliko ya tabia nchi ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa gesi joto katika sekta ya misitu, mkataba huo uliosainiwa katika mkutano uliofanyika nchini Indonesia mwaka 2008.

“Gesi joto ni mchanganyiko wa gesi mbali mbali zinazozalishwa kutokana na shughuli anazofanya binadamu kama vile viwanda, kilimo, sekta ya usafirishaji, magari, na mitambo inayotoa gesi mbalimbali ambayo hupanda hadi kufikia umbali wa kilometa moja hadi moja na nusu kutoka uso wa dunia na huko hutengeneza utando mzito (tabaka la gesi joto)”, alisema Dkt Ningu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...