Sekta
ya ardhi nchini ni ya kipekee katika uthibiti wa mabadiliko ya tabia nchi kwa
kuwa ndiyo sekta pekee ambapo ndipo uzalishaji na uondoaji wa kaboni hutokea.
Mfumo
wa matumizi mapana ya ardhi ambao siyo endelevu unapaswa ubadilishwe ili nafasi
yake ichukuliwe na matumizi ambayo ni sahihi na endelevu zaidi tofauti na hali
ilivyokuwa mwanzo. Hatua hiyo ni pamoja na kutumia vyema ardhi iliyopo kwa
kupunguza uzalishaji wa gesi joto unaotokana na ardhi.
Mnamo
mwaka 2009, Ubalozi wa Ufalme wa Norway nchini Tanzania ulianza kuwa chachu ya uhifadhili
wa miradi saba ya majaribio ya Mkakati wa Kupunguza Ukataji Hovyo na Uharibifu wa Misitu (MKUHUMI) kwa kutoa dola
za Kimarekani zipatazo milioni 100 kufadhili mradi huo.
Fedha
hizo zilipelekwa kwenye taasisi za elimu ya juu nchini ambazo zinajukumu la
kuandaa wataalamu mbalimbali.
Taasisi
zilizopata fedha hizo ni pamoja na Chuo Kukuu Cha Kilimo cha Sokoine (SUA) kwa
lengo la kuendesha mafunzo na utafiti.
Fedha
nyingine zilipelekwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, kitivo cha Tathmini ya
Rasilimali ambako huko pia waliingia mkataba na Asasi zisizo za Kiserikali (NGO’s)
za hapa nchini ili kutekeleza mkakati wa MKUHUMI vijijini.
Mkurugenzi
wa Idara ya Mazingira, Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt Julius Ningu hivi karibuni
alibainisha kuwa MKUHUMI ni moja ya maeneo ya utekelezaji wa mkataba wa
mabadiliko ya tabia nchi ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa gesi joto katika
sekta ya misitu, mkataba huo uliosainiwa katika mkutano uliofanyika nchini
Indonesia mwaka 2008.
“Gesi
joto ni mchanganyiko wa gesi mbali mbali zinazozalishwa kutokana na shughuli anazofanya
binadamu kama vile viwanda, kilimo, sekta
ya usafirishaji, magari, na mitambo inayotoa gesi mbalimbali ambayo hupanda
hadi kufikia umbali wa kilometa moja hadi moja na nusu kutoka uso wa dunia na huko
hutengeneza utando mzito (tabaka la gesi joto)”, alisema Dkt Ningu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...