Mshindi wa shindano la muziki la Airtel Trace Music Stars Afrika Nalimi Mayunga anatarajiwa kuondoka nchini jumatatu ya tarehe 16 novemba kwenda Marekani kwaajili ya mafunzo na kurekodi single yake na mwanamuziki Nguli Duniani, Msenegal Akon.

Mayunga aliibuka kuwa mshindi wa Airtel Trace Afrika katika mashindano yaliyoshirikisha nchi 13 barani Afrika yaliyofanyika nchini Kenya mwanzoni mwa mwaka huu na kujishindia zawadi nono ikiwemo deal ya kurekodi wimbo na video pamoja na kupata mafunzo ya mzuki kutoka kwa mwana muziki Akon nchini marekani.

Akiongea na waandishi wa habari, Afisa Uhusiano wa Airtel Bwana Jane Matinde alisema" Tunajisikia furaha kuwawezesha vijana wa kitanzania kupata fulsa na kufikia ndoto zao kupitia program zetu mbalimbali ikiwemo hii ya Airtel Trace Music Stars. tunajivumia kumuwezesha Mayunga na kumpatai fulsa ya kujinoa kimuziki lakini pia kutanganza nchi yetu na muziki wetu ulimwenguni.

Ni matumaini yetu kuwa , program hii itamuwezesha mayunga na vijana wengine watakao pata nafasi ya kushiriki kubadilisha maisha yao na kuwa wanamuziki bora ndani na nje ya nchi na kuweza kutumia vipaji vyao kama mtaji katika kuendesha maisha yao na famila zao kwa ujumla Kwa upande wake Nalimi Mayunga aliwashukuru Airtel kwa kumpatia nafasi hii ya pekee na kuhaidi kutumia fulsa hii vyema.

"kwangu huu ni muujiza wa pekee kupata nafasi ya kurekodi wimbo na kupata mafunzo toka kwa Akon, nawashukuru sana Airtel kwani mimi binafsi nisingeweza kuonana na Akon lakini kwa kupitia program hii na ushindi nilioupata sasa naondoka kwenda kunolewa na kupata ujuzi toka kwa Akon. Natoa wito kwa vijana wenzangu kutokata tamaa katika kufikia ndoto zao na kushirikia katika mashindano kama haya pindi yanapotangazwa kwani nao wanaweza kupata nafasi kama mimi leo Nimejiandaa vyema kuwakilisha nchi yangu na kurekodi single yangu na Akon hivyo naomba watanzania waendelee kuniunga mkono ili niweze kuwa mwanamuziki nyota duniani.

Kufatia ushindi huo Airtel na Trace imesamwezesha mayunga kurekodi single yake nchi South Afrika ijulikanayo kama " nice couple" nyimbo hii inapatikana youtube na pia inapigwa katika vyombo mbalimbali vya habari.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...