Dr Yash Gulati, 
Senior Spine and Joint Replacement Surgeon 
at Apollo Hospitals; Delhi
Na Mwandishi Wetu,

Maendeleo katika njia za ufanyaji kazi pamoja na matumizi ya teknolojia yanavyokuwa kwa kasi yanaweza kutufanya tuamini tumepunguza maumivu katika viungo vyetu vya mwili ila si hivyo. Tunatumia magari, mitandao mbalimbali ambayo vizazi vilivyopita havijawahi kuota kutumia. Mabadiliko haya mapya katika maisha yetu yenye msisitizo mdogo katika uimarishaji wa viungo umechukua hatamu na kuathiri maisha yetu kwa maana mwili wa binadamu ni ule ule toka miaka milioni iliyopita. Na hiyo inasababisha kuongeza matukio mengi ya maumivu ya mgongo kwa sababu uti wa mgongo umekwisha athirika.

Watu wengi lazima wakutwe na maumivu ya uti wa mgongo walau mara moja katika vipindi vya maisha yao. Sehemu kubwa inayoathirika katika uti wa mgongo ni sehemu ya chini kabisa na sehemu ya shingoni kwa sababu sehemu hizo ndizo zina beba uzito mkubwa wa mwili kila siku. Sababu nyingine zinazosababisha maumivu ya mgongo ni kuharibika kwa diski, mgandamizo katika vertebra na kudhoofika kwa mifupa kutokana na upungufu wa tishu (osteoporosis) kutokana na umri inaweza kusababisha mgandamizo wa vertebra na kusababisha ufa.

Zipo zaidi ya sababu 100 zinazoweza kusababisha maumivu ya mgongo upande wa chini; matukio ambayo yanaweza kusababisha maumivu mgongoni na yasitambulike. Sababu maalumu ya kuleta maumivu ya mgongo inabaki kuwa ni kuharibika au kuvunjika kwa sehemu zinazounga uti wa mgongo kutokana na pozi baya la ukaaji.

BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...