Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Hamad Masauni wa pili kushoto akipokelewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Mbarak Abdulwakil wa watatu kulia mara baada ya Naibu waziri huyo kupokea Ua alilokabidhiwa na watumishi wa wizara hiyo ikiwa ni ishara ya kukaribishwa wizarani hapo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kumuapisha kushika wadhifa huo Ikulu jana jijini Dar es Salaam.
Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Hamad Masauni wa kwanza kushoto akisalimiana na Kamisha wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi Paul Chagonja wa pili kulia muda mfupi baada ya Naibu waziri huyo kukaribishwa wizarani hapo baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kumuapisha kushika wadhifa huo Ikulu jana jijini Dar es Salaam wa kwanza kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).
Naibu waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mh. Hamad Masauni wa pili kushoto akisalimiana na Kamisha wa Utawala na Fedha wa Jeshi la Magereza Gaston Sanga wa pili kulia muda mfupi baada ya Naibu waziri huyo kukaribishwa wizarani hapo mara tu baada ya kuapishwa Ikulu jana jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...