Meneja Uendelezaji wa Biashara wa Benki ya NBC, Eddie Mhina (kulia), akizungumza na baadhi ya wateja wa benki hiyo kuhusu huduma za kibenki zinazofuata kanuni na misingi ya kiislamu (Islamic Banking) katika warsha ya siku moja waliyowaandalia wateja wa NBC mkoani Mtwara hivi karibuni.
Mkuu wa Kitengo cha Huduma za Kibenki zinazofuata misingi ya Kiislamu (Islamic Banking), cha Benki ya NBC, Yassir Masoud (kulia), akielezea kuhusu huduma hizo wakati wa warsha ya siku moja waliyowaandalia wateja wa NBC mkoani Mtwara hivi karibuni.
Meneja Uendelezaji wa Biashara wa Benki ya NBC, Eddie Mhina (kulia), akiagana na mmoja wa wateja wao Mohamed Kioze mara baada ya kuisha warsha ya siku moja waliyowaandalia wateja wa NBC kwa ajili ya kuwaelezea kuhusu bidhaa mbalimbali zinazopatikana kupitia kitengo cha Islamic Banking cha NBC, mjini Mtwara hivi karibuni.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...