Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Bw. Said Meck Sadick akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani ofisini kwake leo alipokutana nao kuelezea utekelezaji wa maagizo aliyoyatoa kwa DAWASCO kuhusu usambazaji wa maji safi na salama ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.
Afisa Mtendaji Mkuu wa  DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja akiongea na waandishi wa habari hawapo pichani Dar es salaam  leo alipokutana nao kuelezea utekelezaji wa maagizo yaliyotolewa na  Serikali kuhusu usambazaji wa maji safi na salama ili kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.Picha zote na Ally Daud-Maelezo.


NA ALLY DAUD-MAELEZO

Shirika la Maji Safi na Maji Taka Dar es salaam (DAWASCO) limeongeza uzalishaji na usambazaji wa Maji safi na Salama kwa wakazi wa jiji hilo hadi kufikia mita za ujazo 280,000 kwa siku ili kubabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu  uliolikumba jiji hilo hivi karibuni. 

Hatua hiyo inatokana na utekelezaji wa maagizo ya Serikali yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadiki kuitaka DAWASCO kusambaza maji safi na salama kwa wakazi wa jiji hilo ili kupambana na Ugonjwa wa Kipindupindu.

Akiongea na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam Mkuu wa mkoa huo Bw. Sadick amesema kuwa kufuatia maagizo aliyoyatoa kwa shirika hilo ikiwemo kusambaza maji safi na salama kwa wananchi pamoja na kutengeneza mifereji ya kupitsha maji taka ili yasiingiliane na mikondo ya maji safi, DAWASCO wametekeleza kwa kiasi kikubwa maagizo hayo.

“Dawasco imehakikisha inazalisha maji safi na salama kati ya mita za ujazo 270,000 na 280,000 kila siku kwa muda wote tangu mlipuko ulipotokea na imehakikisha inasafisha na kusambaza kwa wananchi yakiwa katika viwango vya ubora unaokubalika kwa ajili ya matumizi kwa binadamu” amesema Bw. Sadick.

Ameongeza kuwa Dawasco imejenga vizimba vya maji  safi na salama kwenye maeneo mbalimbali ambayo hayajakumbwa na yaliyokumbwa na athari za mlipuko wa ugonjwa huo kwa jumla ya vizimba 48 ambavyo maeneo ya Kinondoni vizimba 5, Magomeni vizimba 38 na Ilala vizimba 5.

Aidha, amesema kuwa DAWASCO kwa kushirikiana na Ofisi ya Bonde Wami Ruvu imeanza kazi ya kusajili na kuwatambua watu binafsi wenye visima virefu vilivyopo kisheria ambao wanauza maji kwa wananchi ili kuvitambua na kudhibiti ubora wa maji na bei yake ambapo zoezi hili litaendelea hadi Machi 2016.

“Dawasco imefanya jitihada za kuweka dawa ya kuua wadudu aina ya chrolination kwenye maboza  wakati wa  usajili kabla ya kuruhusiwa kufanya biashara ya kuuza maji kwa wananchi na kuongeza sehemu za kuchota maji kwa kuwapelekea wananchi huduma hiyo wakitumia magari yenye matanki yaliyokuwepo kutoka 12 mpaka kufika 49 kwa sasa” aliongeza Bw.Sadick.Katika hatua nyingine Bw. Sadick alitoa rai kwa wakazi wa jiji hilo kuendelea na tabia ya kufanya usafi mara kwa mara ili kutokomezakabisa ugonjwa wa kipindupindu kwani kuanzia juzi hakuna wagonjwa waliopokelewa katika vituo vyote.

Kwa upande wa Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja alisema kuwa wako katika hatua za mwisho kukamilisha ujenzi wa mifereji ya kupitisha maji machafu ili isiingiliane na maji safi kwa wiki mbili zijazo.

“kufikia Februari mwakani tutaweza kutoa maji safi na salama ya kutosha kwa wananchi  wote wa Dar es salaam bila ya matatizo yoyote” alisisitiza Mhandisi Cyprian.   

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Waheshimiwa na watendaji;

    Kwa heshima na taadhima isiwe tu usambazajiwa wa maji safi pia iwe utoaji wa maji taka katika jiji hili na miji mingine hapa Tanzania. Tuondoleeni maji taka tafadhalini. Kipindupindu kipo na kitakuwepo tu iwapo hamtatusaidia kuyaondosha na kuyaelekeza mbali na makazi ya watu maji taka haya. Tafadhalini na tafadhali Mkuu na watendaji wengine tutoleen maji taka mitaani mwetu. Kwa heshima na taadhima tunakuombeeni.

    Mrs. B.S, Kibondo

    ReplyDelete
  2. tunaomba mje na suluhisho la uchafu kwanza mtunge sheria za kutubana sisi wananchi hasa wanaofanya kwa makusudi kutupa takataka watakavyo hasa wewe mkuu wa mkoa kumbuka wewe cheo chako ni kama rais wa mkoa so kua mbunifu kama rais wetu Magufuli sio unasubili mpaka maagizo yatoke serikalini wewe unabanwa na wewe wabane la sivyo utaishia njiani kwa kasi ya Magufuli #hapakazitu

    ReplyDelete
  3. Tangazeni tender za kusomba taka kwa private entities.tender zizingatie uwezo wa makampuni hayo kufanyakazi hizo na siyo sura au majina..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...