Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO , Mhandisi Cyprian Luhemeja akishirikiana na wafanyakazi wa DAWASCO katika zoezi la usafi kwenye soko la Kariakoo katika maadhimisho ya siku ya Usafi kitaifa.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Mecky Sadick pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja wakiendelea na zoezi la usafi.

Shirika la majisafi na majitaka Dar es salaam(Dawasco) katika kutekeleza agizo la mh. Rais john pombe magufuli la kuadhimisha sherehe za uhuru kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali, leo DAWASCO imefanya usafi katika soko kuu la kariakoo lilipo wilaya ya ilala, jijini Dar Es Salaam, ikiwa ni jitihada za kupambana na ugonjwa wa kipindupindu ulioenea nchi nzima.

Usafi huo uliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mh Mecky Sadick pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa DAWASCO Mhandisi Cyprian Luhemeja ulifanya usafi katika maeneo yote muhimu ikiwemo sokon Shimoni, Mtaa wa Msimbazi na Uhuru pamoja na uzibuaji wa Mitaro ya Majitaka katika Mitaa ya Libya na Zanaki.

Akiongea katika usafi huo Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam alisema usafi ni jukumu la kila mwananchi bila kujali itikadi yake na hivyo kuwahimiza wananchi kuwa na tabia ya kufanya usafi katika maeneo yao kuliko kusubiri kupewa maagizo na serkali.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa DAWASCO alisema siku hiyo wameiadhimisha kwa kufanya usafi katika soko la Kariakoo ambalo ni moja ya wateja wake ili kuwa mfano mzuri kwa wananchi na jamii nzima inayohudumiwa na Soko hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...