Mwandishi Wetu
VINARA wa Ligi Daraja la Kwanza katika kundi (A)
klabu ya Friends Rangers, imesajili wachezaji wanne
ambao Emanuel Gabriel, Fred Cosmas, Mussa John
'Rooney' na Ramadhan Chombo 'Redondo' kwa ajili ya
mzunguko wa pili wa Ligi hiyo unaotarajia kuanza hivi
karibuni.
Ofisa Habari wa klabu hiyo Asha Kigundula, alisema
kuwa katika kuhimalisha kikosi chao, wameamua
waongeze wachezaji wanne ambao watasaidia
kupandisha timu yao.
Kigundula alisema kuwa hata hivyo kikosi chao
kitaenda kuweka kambi ya wiki moja Lushoto mkoani
Tanga, kama sehemu ya maandalizi ya mzunguko wa
pili.
Alisema kuwepo kwa wachezaji hao ambao waliwahi
kuvituzimikia klabu kubwa hapa nchini kutasaidia
kujenga zaidi kikosi chao ambacho kimekuwa moto
wa kuotea mbali.
Alisema katika msafara huo jumla ya watu 40,
wataenda katika kambi hiyo maalum, kikiongozwa na
Katibu Mkuu wa timu hiyo na Heyry Chibakasa (Herry
Mzozo).
Rangers yenye maskani yake magomeni Kagera Dar
es Salaam, ndiyo wanaoshika usukani wa Ligi Daraja
la kwanza katika kundi A.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...