Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye akisisitiza jambo wakati wa kikao na wahariri wa magazeti ya Raia Mwema na Raia Tanzania.

  Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM Taifa Ndugu Nape Nnauye akizungumza huku Mhariri Mkuu wa Magazeti ya Raia Mwema na Raia Tanzania Ndugu Godfrey Dilunga akimsikiliza kwa makini.
Mhariri Mkuu wa Magazeti ya Raia Mwema na Raia Tanzania Ndugu Godfrey Dilunga akiwatambulisha baadhi ya viongozi wa kampuni ya Magazeti ya Raia Mwema.

KATIBU wa NEC (CCM) Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye leo ametembelea ofisi za kampuni ya Raia Mwema inayotengeneza magazeti ya Raia Mwema na Raia Tanzania, kwa lengo la kushukuru na kueleza mikakati ya chama chake
.

Itakumbukwa miezi kadhaa iliyopita kabla ya uchaguzi mkuu Nape, alitembelea vyumba vya habari akianzia na Raia Mwema kueleza pamoja na mambo mengine namna walivyojipanga na uchaguzi ikiwemo kupata mgombea urais.

Akizungumza jana katika ofisi hizo alipokutana na wahariri pamoja na viongozi mbalimbali wa kampuni hiyo alisema, wanafurahishwa na kasi ya Rais John Magufuli, kwa sababu kinachotendeka sasa walikipanga hata kabla ya uchaguzi.

“Tulitaka mtu wa aina hii, haya mabadiliko tuliyarataji hivyo hatushituki kuyaona, tunachotaka kuwaambia wananchi tu ni kuwa baada ya kumaliza serikalini mabadiliko yatahamia kwenye chama,” alisema Nape.  



BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...