Na Mathew Mndeme
Tunamshukuru Mungu kwamba Rais kateua mawaziri na serikali imeanza kazi rasmi. Kila waziri kwa sehemu yake ameonesha kwamba ana hamasa na motisha ya kufanya kazi na kwa mara ya kwanza (huenda tangu nipate akili) tumeshuhudia mawaziri wakianza kazi lisaa limoja baada yakuapishwa huku kukiwa na habari kwamba h
Hii ni njema sana na ni dalili nzuri katika kujenga Tanzania mpya inayothamiawa kunywa hata juice walizoandaliwa kwenye ukumbi wa kuapishwa. 
Ni kazi na utumishi kwa wananchi badala ya wanaopewa uongozi kujiona ni miungu-watu, kuona nafasi zao ni za kula bata, na kujinufainya wenyewe na wanaowazunguka. Ninashawishika kwamba, kwa kiwango cha uwajibikaji walichokiweka Rais na Waziri Mkuu (high standard), hakuna waziri atakayelala wala kushindwa kazi kwa visingizio. Hata wale wanaodhaniwa kwamba “sio wazuri sana” katika nafasi walizopewa, nashawishika kwamba watafanya kazi tu hata kama ni kwa kujifunza upya.

Pamoja na kukiri huku, ninaona hatari mbele iwapo mawaziri hawa, ambao wengi katika nafasi walizopewa ni wanasiasa na sio wataalamu, watafanya maamuzi au kutoa maelekezo kwa haraka, bila kuwa na taarifa sahihi kuhusu jambo husika. 

Ninasema hivi kwa sababu baadhi ya mambo ni ya kitaalamu na yanahitaji taaluma husika katika utekelezaji wake hivyo maelekezo yanapotolewa kwamba yafanyike kwa siku/wiki/miezi kadhaa, ni kinyume kabisa na uhalisia.   
Uwezekano wa kufanyika makosa unatokana na ukweli kwamba wakuu wa idara/taasisi/mamlaka wanaoelekezwa kutekeleza haya maagizo, wengi wao wanaonekana kuna na hofu na kutetemeka na kila maagizo wanayapokea tu na kuitikia bila kuwaonesha viongozi wao kwamba mengine hayatekelezeki kwa muda au mtindo wanaotaka wao. 
Mtaalamu yeyote yule katika nafasi yake, lazima awe na uwezo wa kujiamini na kutetea utalaamu wake ikiwa ni pamoja na kusema ukweli kwa kinachoagizwa mbele ya yeyote. 
Sidhani kama kumweleza Rais, Waziri Mkuu, Waziri, au Naibu waziri, kwamba jambo hili uliloagiza linahitaji kuangaliuwa kitaalamu kabla ya kuchukua maamuzi ni kukosa nidhamu au kutokutii. 
Ni bora ujibu kilicho sahihi uadhibiwe (sina hakika kama watafanya hivi) kuliko kuitikia tu halafu ukashindwa au ukaenda kufanya maamuzi ya ajabu ya kitaalamu. Ngoja nitoe mifano miwili:


Kuendelea kusoma Makala hii BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Mambo ya kuheshimiana, kuogopa ogopa watu, kufuata taratibu na michakato ndio yaliyotufikisha hapa. Hata kama hatua za 'hapa kazi tu' zitakuwa na madhara, nadhani adhari zake zitakuwa ndogo kulinganisha na madhara ya uzembe, ubadhilifu na ufisadi uliokidhiri unaofanya pengo la masikini na tajiri tanzania liendele kuongezeka.

    Watanzania tunawafahamu. Mara nyingi bila shuruti au kuogopa hawaendi. Nasubiri tu Mheshimiwa rais etembelee na TAKUKURU, maana siridhiki na utendaji. Kama wameshindwa kuambana na rushwa kutokana na sheria iliyoko, wana mbinu gani mbadala? Wameona hatua za hivi karibuni za kupambana na ufisadi jirani Kenya?

    Speaking of development dictators? Yes, I support 100%.

    ReplyDelete
  2. Mambo ya kuheshimiana, kuogopa ogopa watu, kufuata taratibu na michakato ndio yaliyotufikisha hapa. Hata kama hatua za 'hapa kazi tu' zitakuwa na madhara, nadhani adhari zake zitakuwa ndogo kulinganisha na madhara ya uzembe, ubadhilifu na ufisadi uliokidhiri unaofanya pengo la masikini na tajiri tanzania liendele kuongezeka.

    Watanzania tunawafahamu. Mara nyingi bila shuruti au kuogopa hawaendi. Nasubiri tu Mheshimiwa rais etembelee na TAKUKURU, maana siridhiki na utendaji. Kama wameshindwa kuambana na rushwa kutokana na sheria iliyoko, wana mbinu gani mbadala? Wameona hatua za hivi karibuni za kupambana na ufisadi jirani Kenya?

    Speaking of development dictators? Yes, I support 100%.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...