Na  Bashir  Yakub
Makubaliano  ni  sehemu  ya  maisha  yetu  ya  kila  siku.  Shughuli  zetu  za  kila siku  hutegemea  makubaliano.   Ukimkuta  mtu  anabeba  zege  kwa  ajili  ya  ujenzi  yupo  katika  makubaliano. Ukimkuta  mtu  anaendesha  daladala, bodaboda   yupo  katika  makubaliano. 
Ukimkuta  mtu  katika  ofisi  yoyote  ya  umma  yupo katika  makubaliano,walio kwenye  ndoa  na  uchumba nao  ni  makubaliano,  mfanyakazi  wa  ndani  yupo katika  makubaliano.  Aliyechukua  mkopo,  aliyeuza, kununua  nyumba au  kifaa  kingine  chochote  nao  wote  wapo  katika  makubaliano. Haraka  utaona kuwa  makubaliano  hubeba  sehemu  kubwa  ya  maisha yetu  ya  kila  siku.
Yatutosha  kusema  kuwa  makubaliano  ndio  maisha  yenyewe haswaa.Hata  biashara  yoyote  unayoshirikiana  na  mwenzako  nayo  bila  shaka ni  zao  la  makubaliano. Tutaona hapa makubaliano  yenye  hadhi  ya  kuitwa  mkataba na  ikiwa  mkataba  wa  maneno  unakubalika.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...