Jumuiya ya Wazanzibari waishio nchini Marekani (ZADIA) inapenda kuwaarifu Wazanzibari, Watanzania na Wapenda Amani wote ulimwenguni kuhudhuria katika maandamano ya kushinikiza kumaliza mchakato wa kuhesabu kura na kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika huko nyumbani Zanzibar tarehe 25/10/2015.
Maandamano hayo yatafanyika siku ya Ijumaa tarehe 18/12/2015 kwenye viunga vya Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa, New York kuanzia saa nne asubuhi (10:00 AM) hadi saa sita mchana (12:00 PM). Kufika kwenu kwa wingi na kwa wakati ndio mafanikio ya maandamano yetu haya.
Yoyote atakaesikia taarifa hizi anaombwa amuarifu mweziwe.
Asanteni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Mujitayarishe kurudi kwenu,Donald Trump anashinda urais mwakani,because you are all Isis sympathizers,hamna lolote.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...