Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akizungumza jambo wakati wa ziara yake kwenye kituo cha kuzalisha umeme cha Kidatu. Katikati ni Meneja wa Kituo hicho cha Kidatu, Mhandisi Justus Mtolera na anayemfuatia ni Meneja wa Kituo cha kuzalisha umeme cha Mtera, Mhandisi Abdallah Ikwasa.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akimsikiliza Meneja wa Kituo cha Kuzalisha Umeme cha Kidatu cha Mkoani Morogoro, Mhandisi Justus Mtolera wakati wa ziara yake kituoni hapo lengo likiwa ni kujionea uzalishaji umeme wa kituo hicho.
Bwawa la maji la kuendeshea mitambo ya kuzalisha umeme la Kidatu likionekana katika hali ya kupungukiwa na maji.
Serikali imeagiza matoleo ya maji ya kumwagilia mashamba yanayotumia maji ya mito inayotiririsha kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme ya Mtera na Kidatu yafungwe.
Agizo hilo limetolewa leo na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alipotembelea Bwawa la Kidatu na kujionea namna ambavyo kina cha maji kwenye bwawa hilo kilivyopungua.
Waziri Muhongo alisema tatizo kubwa la uzalishaji mdogo wa umeme wa maji nchini ni umwagiliaji usio zingatia taratibu za matumizi sahihi ya maji.
Alisema mfumo wa umwagiliaji unaotumika ni wa kienyeji sio wa kitaalamu. "Nimeshuhudia mtu anazuia maji kutiririka kwa kutumia mawe, magogo ama viroba vya mchanga; hii sio sahihi," alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...