Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe akizungumza kwenye kikao cha pamoja kati yake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mhe. Januari Makamba (kulia) leo tarehe 29 Desemba 2015 katika ukumbi wa Selous Makao Makuu ya Wizara ya Maliasili na Utalii  Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuipa majukumu Kamati Maalum ya Wataalam ya kutengeneza andiko maalum litakalotumika kuandaa Programu ya pamoja ya kitaifa ya upandaji miti nchi nzima kuanzia mijini hadi vijijini kwa lengo la kuhifadhi na kuendeleza mazingira ikiwemo misitu. Kwa mujibu wa Prof. Maghembe Kamati hiyo imepewa wiki mbili kukamilisha kazi. Mpango huo utashirikisha pia Wizara ya TAMISEMI.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano Mhe. Januari Makamba (kulia) akizungumza katika kikao hicho. Kushoto ni Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe.
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Prof. Jumanne Maghembe akifafanua jambo katika kikao hicho.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Duuh naona JM wamekupunguzia kasi. Foreigh Affairs ndio ingekufaa ujinoe ila sasa naona unapata uzoefu wa kupanda miti.

    ReplyDelete
  2. Kwa maoni yangu mazingira tuyajuayo sisi ni pamoja na mitaa tunayoishi sisi wananchi wakawaida. Tafadhalini wadau na watoa maamuzi mtusikilize sisi wananchi wa kawaida tunakerwa na maji taka yanayochafua mazingira. Hebu tafadhalini waheshimiwa wote haya mazingira yetu yenue Waziri special tuangalizieni na mutusafishie. tuko tayari kuendeleza usafi na infrastructure mtakazotuwekea. Mumejenga mitaro yamajitaka, haifanyi kazi inatirirsha majimachafu mabarabarani.Tafadhalini watoto wetu nasi wenyewe tunatembea kwenye vinyesi na uchafu. Ni aibu yetu sisi wenyewe. Magari ya taka hayapiti mitaani na taka simetujaalia huku manyumbani mwetu. Tafadhali Waziri wa Mazingira na Waziri unayehusika na Mitaa kuweni serious. Nyinyi mmesafika na kuzungumzia mazingira ya miti na misitu,TUTAZAMIENI MITAA YETU. Hata hilinalotumngojee Mheshimiwa rais aseme au amfukuze mtu kazi? Tafadhalini jamani.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...