SHIRIKA la ndege la Etihad, ndege rasmi ya taifa za Falme za kiarabu na Cognizant (NSADAQ: CTSH), shirika linaloongoza kwa huduma za teknolojia ya habari, ushauri na biashara, leo wametangaza makubaliano ya kimkakati yatakayoendesha mabadiliko ya kidijitali pande zote za shirika hilo pamoja na washirika wake.

Chini ya mpango wao wa miaka mitatu wenye thamani ya mamilioni ya madola, Cognizant watawasaidia Etihad kufafanua mkakati wao wakidigitali na kutengeza dhana mpya ambayo itatumika katika kutoa huduma bora kwa wageni wao watakaosafiri popote na ndege za Etihad.

Kwa kuleta pamoja mikakati ya kidijitali, teknolojia, sekta na uzoefu wa ubunifu, Cognizant watafanya utafiti wa hali ya sasa ya biashara na teknolojia ya shirika la ndege la Etihad na kutumia utafiti huo kutengeneza mazingira ya kidijitali ya kiwango cha hali ya juu, itakachowezesha usambazaji kupitia idhaa nyingi, ugawaji wa wateja kwa kina zaidi na kubinafsisha ujuzi katika masoko.

Kwa kutumia taarifa mbalimbali na ufahamu wa mteja, Cognizant italiwezesha shirika la ndege la Etihad na washirika wake, kuelewa zaidi mahitaji ya wageni wake.
Kusoma zaidi bofya HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...