Mwenyekiti wa Taifa wa Shirikisho la Vyama Watu wenye Ulemavu Tanzania(SHIVYSWATA) Amon Anastaz Mpanju akizungumza na wandishi wa habari hawapo pichani juu ya kumpongeza  Rais   John Pombe Joseph Magufuli kwa kutimiza ahadi yake ya kuyajali  na kuyapa kipaumbele masuala ya watanzania wenye ulemavu kwa uteuzi wa Naibu Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera,Bunge,Kazi Vijana na Ajira  Dk.Abdallah Possy, kulia ni Mwekahazina Alias Masamaki
 Waandishi wa habari wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taifa wa Shirikisho la Vyama Watu wenye Ulemavu Tanzania(SHIVYSWATA) Amon Anastaz Mpanju.(picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii).
 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
SHIRIKISHO la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (Shivyawata), limesema kuwa changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu nchini ni ukosefu wa mazingira rafiki  ya kupatia elimu kwa jamii hiyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Shivyawata , Amon Mpanju amesema kuwa kwa serikali ya awamu ya tano iweke mkazo katika mazingira ya watu wenye ulemavu ikiwemo na upataji wa habari kwa kundi la watu wasiosikia.


Mpanju amesema kuwa watu wenye ulemavu wamekuwa na sera lakini hajawahi kutekelezwa katika serikali zilizopita hivyo kwa serikali ya awamu ya tano  itekeleze sera kwa vitendo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...