Familia ya marehemu Mwalimu Ngore N. Kondo wa Chang’ombe, Dar es salaam tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa ndugu, jamaa na marafiki walioshirikiana nasi kwa kutufariji kwa hali na mali katika kumuuguza mpaka kumzika baba yetu mpendwa aliyefariki tarehe Novemba 28, 2015 katika hospitali ya Regency na kuzikwa tarehe Novemba 29, huko  Chamazi.

  Shukrani za pekee ziwafikie Madaktari, Wauguzi na Wafanyakazi wa hospitali za Hindu Mandal na Regency za hapa DSM. Pia shukrani ziwafikie Uongozi na wafanyakazi wa Chuo cha Watumishi wa Umma (Magogoni) ambapo marehemu alifanya nao kazi kwa zaidi ya miaka thelathini (30). Na pia shukrani ziwafikie Uongozi na wafanyakazi wa Benki Kuu ya Tanzania, Hospitali ya Aga Khan pamoja na Kinondoni 'B' Dispensany & Medical consultant na Benki ya NMB ambako watoto wa marehemu Hadija, Nasra na Abdul ni watumishi wa taasisi hizo.
  Ni vigumu kuwashukuru wote kwa majina.  Tunawashukuru wote, ndugu, jamaa, marafiki na majirani wa Chang’ombe na Chamazi kwa ushirikiano wenu mkubwa.
  Tunapenda pia kutumia nafasi hii kuwataarifu na kuwakaribisha katika shughuli ya arobaini na hitma ya marehemu baba yetu mpendwa itakayofanyika Jumapili ya tarehe 3 Januari, 2016 saa sita mchana nyumbani Chang’ombe.

  Inna Lillahi wa inna ilayhi Rajiun 
“Hakika, sisi ni wa mwenyezi mungu 
na hakika kwake tutarejea” – Quran 2:156

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Mwalimu wetu masikini, pole Hadija, pole wote

    ReplyDelete
  2. Tupo pamoja Kapilino na Nasra.Apumzike mahala pema

    ReplyDelete
  3. Inna Lillahi wa Inna Ilayhi Rajiun, Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema pepon Amen.

    ReplyDelete
  4. Mwassy MussaDecember 29, 2015

    poleni wanafamilia hakika pengo lake kuzibika ni vigumu innalilahi wainnailahi rajiun pumzika kwa amani mwalimu wa mikato Mr. Kondo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...