Na Jacquiline Mrisho na Nyakongo Manyama -MAELEZO
SERIKALI ya Tanzania imesaini mikataba miwili na Serikali ya Uswisi ili kuendeleza na kuimarisha huduma za kijamii nchini hasa katika Sekta ya Afya.
Akizungumza na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salam Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Dkt. Servacius Likwelile amesema kuwa kupitia ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo mbili, Serikali ya Uswisi inaendelea kusaidia kuboresha Sekta ya Afya nchini hususani kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
“Uswisi imesaidia Sekta ya Afya kwa miaka 15 na mpaka sasa imeshachangia jumla ya shilingi billion 181.7 kuanzia miradi ya afya ianzishwe nchini” alisema Likwelile.
Aidha, Dkt. Likwelile aliongeza kuwa Serikali ya Uswisi imelenga pia kusaidia kuimarisha utoaji wa huduma katika idara ya Afya katika Serikali za Mitaa kwa kuzingatia usawa na ubora wa huduma hizo hasa kwa wanawake,watoto pamoja na makundi yaliyotengwa hasa maeneo ya vijijini.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...